Wanasheria kuanza kupandikizwa Chip ya ubongo ili kurahisisha kesi na kupunguza gharama

Ripoti ya Chama cha Wanasheria, shirika la kitaaluma la mawakili nchini Uingereza, limesema kuwa chip ya kompyuta inaweza kupandikizwa kwenye akili za mawakili, jambo ambalo linaweza kupunguza gharama za kesi na kupunguza idadi ya mawakili kutatua kesi ngumu.

Hii itakuwa hatua ya mapinduzi katika sekta ya sheria.

Ripoti hiyo, 'Neuroteknolojia, Sheria na Taaluma ya Sheria', iliandaliwa na Dk Alan McKay kwa ombi la Chama cha Wanasheria cha Uingereza na Wales. Katika ripoti hii, Dk. McKay, anayehusishwa na Shule ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Sydney, Australia, anajadili faida zinazoweza kupatikana za kutumia akili bandia katika taaluma ya sheria au sekta ya sheria. Watetezi wa kuanzisha teknolojia ya neva (neurotechnology) kwa wanasheria wanasema kuwa wateja wa makampuni au wateja wa biashara wanashinikiza chip kama hiyo, wakisema inaboresha utendakazi. Kwa hivyo, mawakili wanaotoza £1,500 kwa saa watalazimika kutoza ada zao kulingana na 'vitengo vya malipo vinavyoweza kutozwa', yaani, muda waliotumia kufanyia kazi au kufikiria kuhusu kesi. Nimetumia muda gani? Kana kwamba watalipwa kulingana na mita iliyounganishwa na ubongo badala ya muda wa kwenye saa. Chama cha Wanasheria, ambacho kinahusika na masuala ya kitaaluma ya wanasheria nchini Uingereza na Wales, kilisema katika ripoti iliyochapishwa hivi karibuni kwamba chip ya ubongo kama hiyo itakuwa 'iPhone ya siku zijazo' kwa sekta ya sheria.

Hakutakuwa na haja ya timu kubwa ya mawakili kushughulikia kesi ngumu, lakini Wakili mkubwa mwenye chip ataweza kupembua maelfu ya nyaraka na maelezo kuhusiana na mambo mbalimbali ya kesi hiyo kwa muda mfupi sana na kutengeneza hoja zake kuu namaoni.

Ada ya kila saa ya wakili imekuwa suala la muda mrefu. Ingawa makampuni ya kimataifa yana ada kubwa ya uanasheria kama sehemu ya biashara, kupunguzwa kwa gharama za kisheria kwa msaada wa teknolojia hakika kutavutia watendaji wakuu wa makampuni haya.

Jumuiya ya wanasheria inasema mawakili watataka kuchukua fursa ya akili bandia kwa kutumia teknolojia ya neva kutoa huduma bora na kupata makali zaidi ya washindani wao.

Kulingana na ripoti hiyo, shinikizo la kupitisha teknolojia mpya litatoka kwa wateja. 'Mtu anaweza kufikiria mabadiliko ambayo teknolojia yenye uwezo wa kutambua umakini au inaweza kuleta umakini. Kwa hivyo, badala ya ada ya saa, ada kwa kila kipindi cha umakini itatozwa.

Dk. McKay anasema kwamba Elon Musk, mtu tajiri zaidi duniani, amekuwa akiwekeza katika teknolojia ya neva kwa miaka minane iliyopita. Alisema kuwa 'teknolojia hizi zinakuja, tunapaswa kufikiri juu ya sheria na kanuni zake.'

Wakili na mwandishi Richard Susskind anasema matumizi ya akili bandia yatakua kwa kasi na baadhi ya mifumo ya akili bandia (IA) tayari imefanya vizuri kwa wanasheria wadogo katika kazi fulani, kama vile kukagua hati. Alisema kuwa 'kwenda mbele, ufanisi wa kidijitali wetu sote utaongezeka.

Swali pekee ni kama mchakato na uhifadhi huu utakuwa ndani au nje ya miili yetu.'