Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Je sanaa ya Cuba inawasilisha vipi mapambano ya ukombozi wa Afrika?
Maonyesho ya vipeperushi vya matangazo ya propaganda za Cuba huko London yanaonyesha msaada ambao Fidel Castro alitoa kwa harakati za ukombozi wa Afrika wakati wa vita baridi.
Kazi za sanaa zilizotengenezwa katika kampuni ya Castro ya mshikamano wa watu wa Asia, Afrika na Amerika ya Kusini (Ospaaal) ambayo ilianzishwa mwaka 1966 huko Havanna katika mkutano wa 'Tricontinental' kwa lengo la kupambana na ukoloni wa Marekani.
"Nchi nyingi za Afrika ziliwakilishwa kama wajumbe katika harakati za ukombozi. Vilevile Castro alisaidia kuwaunganisha baadhi ya viongozi haswa kutoka Guinea-Bissau," Olivia Ahmad, miongoni mwa wachoraji aliiambia BBC.
Cabral aliongoza mapigano dhidi ya ukoloni wa Ureno huko Guinea-Bissau na kisiwa cha Cape Verde, lakini aliuwawa mwaka 1973, mwaka mmoja kabla Guinea-Bissau kupata uhuru.
Bi Ahmad anasema kuwa mkutano ule wa Tricontinental ulikuwa umepangwa kufanyika lakini haukufanyika hivyo ukachapishwa.
Hivyo machapisho yake kuwa kiungo muhimu cha taarifa na uwasilishi.
Mapinduzi ya Amerika Kusini yalijulikana zaidi, Ernesto "Che" Guevara, labda alikuwa mpambanaji zaidi katika harakati hizo.
"Lakini pia kuna viongozi wa kiafrika ambao wamekuwa wakikumbukwa kwa ushujaa wao "
Guevara aliipambania nchi ambayo inatambulika sasa Jamuhuri ya kidemokrasia ya Kongo mwaka 1965 ,kwa dhamira iliyoshindwa ya kuchochea uasi dhidi ya utawala wa kigeni wa miaka minne baada ya kuuawa kwa shujaa wa uhuru wa Kongo, Patrice Lumumba.
Lumumba aliuwawa miezi minne baada ya kuchaguliwa kuwa waziri mkuu wa kwanza kidemokrasia katika taifa lake, jambo ambalo lililaumiwa na wanaintelijensia wa Marekani na Uingereza.
"Michoro hiyo inavutia kwa sababu kwa sababu ya sanaa yake ya ushawishi ambao huwezi kutarajia kuuona, michoro hii ina muonekano wa kuwaenzi kwa furaha watu ambao walijitoa mhanga ili kuleta ukombozi," anasema bi Ahmad.
Maonyesho haya ya picha yaliobuniwa Cuba, yaliandaliwa na wabunifu 33 na wengi wao wakiwa wanawake.
Picha kuhusu Guinea-Bissau inamuonyesha mwanamke akiwa ameshikilia bunduki, huyo ni Berta Abelenda Fernandez, "ni miongoni mwa wanawake ambao walitumiwa katika picha nyingi za Ospaaal", Bi Ahmad alieleza.
Castro alijitoa sana katika taifa la Angola, sio kama kwenye operesheni ya siri ya Cuba barani Afrika ya mwaka 1960s, wakati ambao kulikuwa na fursa nyingi za kujinadi kimataifa kuhusu mshikamano na kuleta mabadiliko kidunia.
Baada ya Angola kupata uhuru wake kutoka kwa wareno mwaka 1975, Castro alituma msaada wa kijeshi kwa kutuma wanajeshi wake 35,000 kusaidia na kusitisha chuki dhidi ya ubaguzi wa rangi huko Afrika kusini , jambo ambalo Marekani lilipanda katika utawala wake.
Inakadiriwa kuwa wacubani wapatao 4,300 waliuwawa katika migogoro ya Afrika, nusu yao waliuwawa nchini Angola peke yake katika mapigano yaliyoisha mwaka 2002.
Picha hizi zinabeba ujumbe wa mshikamano waukombozi .
Picha hizi wameweka maelezo ya lugha nne, kiingereza, kifaransa, kispaniola na kiarabu ili ziweze kuenea katika maeneo mngi zaidi ya Cuba pekee.
Unaweza kusoma pia:
Picha nyingi zimelenga mapambano dhidi ya watu wachache weupe nchi Afrika Kusini , mapambano ambayo yaliweza kutokomezwa mwaka 1994, wakati ambapo Nelson Mandela alipochaguliwa kuwa rais.
Kitabu cha mapinduzi ya Cuba Marekani kilitoa fursa ya kuitangaza ndege ya Afrika kusini na kuijumuisha kwenye mkutano wa 'Tricontinental' wa mwezi Julai -Agosti mwaka 1968 ikitoa ahadi ya kutokomeza ubaguzi wa rangi ambao umesababisha kundi kubwa la waafrika waliopinga ubaguzi kuwekwa gerezani na maelfu ya waafrika wakiwa wanafanyishwa kazi kama watumwa katika migodi na maeneo mengine.
Baada ya Mandela kufungwa gerezani mwaka 1964, ilikuwa ni kosa la jinai nchini Afrika kusini kwa mtu kumpiga picha au kuchapisha picha yake ya zamani . Picha ya mchoro huu ilitolewa mwaka 1989, mwaka mmoja kabla hajatolewa gerezani baada ya kufungwa kwa miaka 27.
Msanii aliyechora picha hiyo alikuwa anakaa Havana na alikuwa anajaribu kutumia uwakilishi wa watu kiuhalisia katika siasa.
Dhana ya mshikamano kimataifa imebadilika na unaweza kuona ni kwa nini?