Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mark Zuckerberg amwambia bintiye kucheza nje
Muanzilishi wa mtandao wa kijamii wa Facebook, tajiri Mark Zuckerberg, amemsihi bintiye mdogo kucheza nje na kufurahia maajabu ya kuwa mtoto, katika barua yenye hisia iliyochapishwa katika ukurasa wa mtandao wake wa kijamii.
Barua hiyo ilichapishwa siku ya Jumatatu alipotangaza kuzaliwa kwa mwanawe wa pili aitwaye August, na mkewe Priscilla Chan.
Katika barua ya kina waliyoiandika, wazazi hao wawili walizungumzia kuhusu maajabu ya kuwa mtoto na umuhimu wa kucheza.
Wawili hao waliweka mtandaoni barua kama hiyo kwa binti yao Max mnamo mwaka 2015.
Maaandishi hayo ambayo inaambatana na picha ya familia katika ukurasa wa Facebook wa Bwana Zuckerberg, kumhimiza mgeni huyo mchanga wala sio "kukua mkubwa haraka".