Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Messi afunga ndoa na mpenzi wake wa utotoni
Nyota wa soka nchini Argentina Lionel Messi amemuoa mpenziwe wa utotoni nyumbani kwao katika kile kilichotajwa kuwa harusi ya karne.
Sherehe hiyo kati ya Messi mwenye umri wa miaka 30 na Antonela Rocuzzo mwenye umri wa miaka 29 ilifanyika katika hoteli ya kifahari katika mji wa Rosario.
Nyota wa soka na watu maarufu walikuwa miongoni mwa wageni 260 huku mamia ya maafisa wa polisi wakipelekwa kushika doria.
Messi na Rocuzzo walikutana wakiwa watoto wa miaka 13 kabla ya yeye kuelekea Uhispania.
Miongoni mwa wageni katika harusi hiyo ya Ijumaa ni wachezaji wenza Luis Suarez, Neymar, Gerrard Pique na mkewe Nyota wa muziki Shakira.
Idadi kubwa ya wageni walisafiri kuelekea Rosario katika ndege za kibinafsi.
Gazeti la Argentina la Clarine limeitaja harusi hiyo kuwa harusi ya mwaka na harusi ya karne.