Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Polisi wafuatilia wahalifu wa misimamo mikali Ufaransa
Waziri mkuu wa Ufaransa Manuel Valls amesema kuwa polisi wanafuatilia watu karibu elfu kumi na tano nchini Ufaransa wanaotuhumiwa kuwa na msimamo mkali.
Valls amewaambia waandishi wa habari kuwa mashambulio kadhaa ya waislamu yamezuiliwa ,amesema mashambulio mawili yalizuiliwa wiki iliyopita.
Polisi walimkamata kijana mmoja nyumbani kwao Paris siku ya jumamosi kwa tuhuma za kupanga shambulio la kisu.