Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Biashara na uwekezaji wasisitizwa katika mkutano wa G20
Mkutano wa mwaka wa G20 unaojumuisha mataifa yenye uchumi mkubwa duniani umemalizika nchini China, ukiongozwa na Rais Xi Jinping, amesema wajumbe wa nchi wanatakiwa kuimarisha nguvu mbili za kibiashara na uwekezaji.
Akiongea huko Hangzhou, Rais Xi amesema kutakuwa na makubaliano kupinga ulinzi wa soko. Amesema kuwa kwa mara ya kwanza mkutano huo umeweka masuala ya maendeleo mbele na kati.
Mkuu wa IMF, Christine Lagarde, amesema viwango vya ukuaji uchumi duniani umekuwa ukishuka kwa muda mrefu na wajumbe wa G-20 watatumia kila njia kuukuza.
Na tamko la mwisho limekubaliana na mataifa kuongeza usaidizi wa ubinadamu na na misaada kwa wakimbizi.