Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 02.10.2018: Mbappe, Pogba, Mourinho, Ramsey, Sanchez, Diop

Chanzo cha picha, Getty Images
Meneja wa Manchester City Pep Guardiola ameka nushataarifa kwamba anataka kumnunua mshambuliaji wa Paris St-Germain Kylian Mbappe, 19. (Independent)
Bodi ya Barcelona imagawanyika kuhusu ikiwa itamwendea kiungo wa kati wa Manchester United Paul Pogba, 25 mwezi Januari lakini mabingwa hao wa Uhispania wanaamini wana uwezo wa kifedha wa kutosha kuweza kumsaini Mfaransa huyo mshindi wa Kombe la Dunia. (ESPN)
Real Madrid wamejiunga katika kundi la klabu zinazomzea mate mchezaji wa kimataifa wa Wales Aaron Ramsey, 27, ambaye atondoka Arsenal mwezi January. (Teamtalk)

Chanzo cha picha, Getty Images
Arsenal ni kati ya vilabu vinavyommezea mate mchezaji wa Lille, Nicolas Pepe, 23.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast mwenye thamani ya pauni milioni 30 amepokelewa vizuri chini Ufaransa kwa mchezo wake mzuri msimu huu baada ya kufunga mabao matano katika mechi nane.

Chanzo cha picha, Getty Images
Chelsea wako katika nafasi nzuri ya kumsaini mchezaji mwenye miaka 15 wa Volendam Mholanzi Sam Lautenschutz. (The Sun)
Wolves wanamwinda mlinzi wa Aberdeen raia wa Scotland Scott McKenna. Ofa za Celtic na Aston Villa zimekataliwa kwa mchezaji huyo mwemye miaka 21. (Scottish Sun)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiungo wa kati wa zamani wa Manchester United Lee Sharpe anaamini meneja wa klabu Jose Mourinho anastahilia kufutwa ikiwa matokeo yao mabaya yataendelea kwa mechi zao mbili wiki hii. (Talksport)
Meneja wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zidane anariptiwa kumpigia simu Mourinho kumhakikishia kuwa hakuna mipango ya kuchukua mahala pake. (Mirror)

Chanzo cha picha, Getty Images
Mourinho anaaminiwa kutengwa huko Old Trafford baada ya kutofautiana na nahodha wa timu Antonio Valencia. (Mail)
Mshambuliaji wa United Alexis Sanchez, 29, alibaki akiteta baada kuachwa nje ya mechi na Mourinho kwa mechi wa wikendi na West Ham. (Mirror)
Mchezaji anayetafutwa na United Sergej Milinkovic-Savic ameongeza mkataba wake na Lazio hadi mwaka 2023. Mchezaji huyo mwenye miaka 23 raia wa Serbia alihusishwa na kuhamia Old Trafford majira ya joto. (Mail)

Chanzo cha picha, Getty Images
West Ham wamewashinda Manchester United, Barcelona, Arsenal, Tottenham na Everton katika kumsaini mlinzi huyo mwenye miaka 21 Issa Diop msimu huu. (Mail)
Kiungo wa kati wa England Danny Drinkwater, 28, hana haraka ya kuondoka Chelsea licha ya kutokuwa kwenye kikosi cha meneja Maurizio Sarri. (Telegraph)
Bora zaidi kutoka Jumatatu
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho ana hofu kuhusu hatma yake huko Old Trafford na anaamini kuwa maafisa wa klabu wamewasiliana na meneja wa zamani wa Real Madrid Zinedine Zidane. (Sun)
Lakini mchezaji huyo wa zamani kimataifa wa Ufaransa analenga kuwa meneja mpya wa Juventus. (Tuttosport, via Daily Express)
Sintofahamu kuhusu hatma ya Mourinho huko United inamaanisha kuwa wachezaji 12 hawana uhakika kuhusu hatma yao wakati wanaingia mwaka wa mwesho wa mikataba yao. (Daily Mirror)

Chanzo cha picha, Getty Images
Mourinho amekosa uvumilivu kwa mshambuliaji raia wa Chile Alexis Sanchez, 29. (London Evening Standard)
Mlinzi wa Manchester United raia wa England Luke Shaw, 23, anasema kikosi kilicheza vibaya wakati kilishindwa na West Ham siku ya Jumamosi. (Daily Telegraph)
Manchester City watangoja kabla ya kumpa ofa mpya kiungo wa kati mwenye miaka 18 Phil Foden ya mkataba mpya wa miaka mitano wa pauni 250,000 kwa wiki. (Daily Star)

Chanzo cha picha, Getty Images
Meneja wa City Pep Guardiola amemuonya wing'a mjerumani Leroy Sane, 22, akitaka asipoteze mwelekeo. (Sun)
Maajenti wa Manchester City, Liverpool na Tottenham walimtazama kiungo wa kati wa Lazio raia wa Serbia Sergej Milinkovic-Savic, 23, wakati wa ushindi wa mabao 4-1 dhidi ya Genoa. (Daily Mirror)












