Golden Boy: Kylian Mbappe, Boubacar Kamara, Phil Foden & Trent Alexander-Arnold kushindania tuzo ya kinda bora duniani

Chanzo cha picha, PA
Mchezaji nyota wa Ufaransa Kylian Mbappe na raia mwenzake Boubacar Kamara wameorodheshwa kushindania tuzo ya mchezaji bora wa umri mdogo barani Ulaya.
Tuzo hiyo ambayo hufahamika kama 'Golden Boy' kwa maana ya Kinda wa Dhahabu imekuwa ikitolewa na gazeti la Italia la Tuttosport mwaka 2003.
Tuzo hiyo hutolewa kwa mchezaji bora zaidi wa chini ya miaka 21 barani Ulaya.
Mshambuliaji wa Paris Saint German Kylian Mbappe ambaye alishinda Kombe la Dunia akiwa na Ufaransa mwezi Julai anapigania kushinda tuzo hiyo kwa mwaka wa pili baada ya kushinda mwaka jana.
Kwa jumla wachezaji 40 wameorodheshwa.
Kwenye orodha hiyo kuwa mchezaji wa Liverpool Trent Alexander-Arnold na nyota wa Manchester City Phil Foden na pia Tom Davies wa Everton na mchezaji aliyenunuliwa na Manchester United mwezi Agosti Diogo Dalot.

Chanzo cha picha, Andrew Powell
Mkabaji kamili Alexander-Arnold, 19, alicheza katika fainali ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya real Madrid mwezi Mei ambao Liverpool walishindwa, na pia alikuwa kwenye kikosi cha England cha Kombe la Dunia kilichotumiwa na meneja Gareth Soutgate.
Foden, 18, bado hajachezeshwa timu ya taifa lakini alikuwa mfungaji mabao bora katika Kombe la Dunia la wachezaji wa chini ya miaka 17 mwaka jana.
Alifunga bao lake la kwanza akichezea Manchester City mechi yao waliyowashinda Oxford katika Kombe la Carabao Jumatano.
Washindi wa awali ni pamoja na Neymar, Edinson Cavani, Lionel Messi, Wayne Rooney na Paul Pogba.
Orodha kamili ya wachezaji wanaoshindania tuzo
1) Trent John ALEXANDER-ARNOLD, LIVERPOOL, West Derby (Liverpool, England), 7 Oktoba 1998, England, Beki
2) Kelvin Adou AMIAN, TOLOSA, Toulouse (Fra), 8 Februari 1998, France-Ivory Coast Beki
3) Houssem AOUAR, OLYMPIQUE LIONE, Lyon (Fra), 30 Juni 1998, France-Algeria, Kiungo wa kati
4) Musa BARROW, ATALANTA, Banjul (Gam), 14 Novemba 1998, Gambia, Mshambuliaji
5) Justin BIJLOW, FEYENOORD, Rotterdam (Ola), 22 Januari 1998, Dutch, Mlinda lango
6) Josip BREKALO, WOLFSBURG, Zagreb (Cro), 23 Juni 1998, Croatia, Mshambuliaji
7) Patrick CUTRONE, MILAN, Como (Italy), 2 Januari 1998, Italia, Mshambuliaji
8) Daniel Carvajal DANI OLMO, DINAMO ZAGABRIA, Terrassa (Spa), 7 Mei 1998, Uhispania, Mshambuliaji
9) Thomas DAVIES, EVERTON, Liverpool (Eng), Juni 30, 1998, England, Kiungo wa kati
10) Matthijs DE LIGT, AJAX, Leiderdorp (Ola), 12 Agosti 1999, Uholanzi, Beki
11) Moussa DIABY, PARIS SAINT-GERMAIN, Paris (Fra), 7 Julai 1999, France-Ivory Coast, Mshambuliaji
12) José Teixeira DIOGO DALOT, MANCHESTER UNITED, Braga (Por), 18 Machi 1999, Ureno Kiungo wa kati

Chanzo cha picha, Getty Images
13) Moussa DJENEPO, STANDARD LIEGI, Bamako (Mli), 15 Juni 1998, Mali, Kiungo wa kati
14) Ritsu DOAN, GRONINGEN, Amagasaki (Gia), 16 Juni 1998, Japan, Mshambuliaji
15) Gabriel ÉDER MILITÃO, PORTO, Sertãozinho (SP, Bra), 18 Januari 1998, Brazil, Beki
16) Odsonne ÉDOUARD, CELTIC GLASGOW, Kourou (Guyana, Fra), 16 Januari 1998, France-Guyana, Mshambuliaji
17) Ferreira da Silva EVANDER, MIDTJYLLAND, Rio de Janeiro (Bra), 9 Juni 1998, Brazil, Mshambuliaji
18) Philip Walter FODEN, MANCHESTER CITY, Stockport (Eng), 28 Mei 2000, England, Kiungo wa kati
19) Achraf Mouh HAKIMI, BORUSSIA DORTMUND, Madrid (Spa), 4 Novemba 1998, Uhispania-Morocco, Beki
20) Amadou HAIDARA, RED BULL SALZBURG, Bamako (Mli), 31 Januari 1998, Mali, Kiungo wa kati
21) Siqueira JOÃO FÉLIX, BENFICA, Viseu (Por), 10 Novemba 1999, Ureno, Kiungo wa kati
22) João Pedro Neves Filipe JOTA, BENFICA, Lisbon (Por), Machi 30, 1999, Ureno, Mshambuliaji
23) Eduardo Borges JOVANE CABRAL, SPORTING LISBON, Assomada (CPV), 14 June 1998, Cape Verde, Mshambuliaji
24) Dejan JOVELJIC, STELLA ROSSA, Bijeljina (Bos), 7 Agosti 1999, Bosnia- Serbia, Mshambuliaji
25) Boubacar KAMARA, OLYMPIQUE MARSEILLE, Marseille (Fra), 23 Novemba 1999, France-Mauritania, Beki
26) Moise Bioty KEAN, JUVENTUS, Vercelli (Ita), 28 Februari 2000, Italia-Ivory Coast, striker
27) Abdoulaye Jules KEITA, DIGIONE, Conakry (Gui), 20 Julai 1998, Guinea, Mshambuliaji
28) Justin KLUIVERT, ROME, Zaandam (Ola), Mei 5, 1999, Uholanzi-Suriname, Mshambuliaji
29) Alban LAFONT, FIORENTINA, Ouagadougou (Buf), 23 Januari 1999, France-Burkina Faso, portierte
30) Manuel Alonso MANU GARCIA, TOLOSA, Oviedo (Spa), 2 Januari 1998, Uhispania, Kiungo wa kati
31) Kylian Sanmi Lottin MBAPPÉ, PARIS SAINT-GERMAIN, Bondy (Fra), 20 Desemba 1998, France-Cameroon, Mshambuliaji

Chanzo cha picha, Michael Regan
32) Pietro PELLEGRI, AS MONACO, Genoa (Ita), Machi 17, 2001, Italia, Mshambuliaji
33) Christian Mate PULISIC, BORUSSIA DORTMUND, Hershey (PA, Usa), Septemba 18, 1998, Marekani-Croatia, Kiungo wa kati
34) Marcelo Josemir Pintos SARACCHI, RB LIPSIA, Paysandú (Uru), 23 Aprili 1998, Italia-Uruguay, Beki
35) Ismaila SARR, RENNES, Saint-Louis (Sen), 25 Februari 1998, Senegal, Mshambuliaji
36) Dayotchanculle Oswald UPAMECANO, RB LIPSIA, Évreux (Fra), 27 Oktoba 1998, France-Guinea, Beki
37) José Paixão de Oliveira VINICIUS JUNIOR, REAL MADRID, San Gonçalo (Bra), 12 Julai 2000, Brazilian, Mshambuliaji
38) Moussa WAGUÉ, BARCELONA, Bignona (Senegal), 4 Oktoba 1998, Senegal, Beki
39) Timothy Tarpeh WEAH, PARIS SAINT-GERMAIN, New York (USA), 22 Februari 2000, France-Marekani, Mshambuliaji
40) Nicolò ZANIOLO, ROMA, Massa (Italia), 2 Julai 1999, Italia, Kiungo wa kati












