Tetesi za Soka Ulaya Jumanne 25.09.2018: De Jong, Herrera, Mourinho, Pogba

Chanzo cha picha, Getty Images
Manchester United na Real Madrid wana mipango ya kumsaini kiungo wa kati wa Ajax Mholanzi mwenye miaka 21, Frenkie de Jong, anayewekewa thamani ya pauni milioni 72. (De Telegraaf - in Dutch)
Kiungo wa kati wa Uhispania Ander Herrera, 29, angetaka kubaki huko Old Trufford licha ya Barcelona kumzea mate. (ESPN)

Chanzo cha picha, Getty Images
Arsenal wanamwinda mchezaji wa Rennes raia wa Senegal mwenye miaka 20 Ismaila Sarr, ambaye pia anatazamwa na Inter Milan.(Mirror)
NewCastle watafanya mkutano na meneja Rafael Benitez kuhusu bajeti ya mwezi Januari kujaribu kumwezesha Mhispania huyo kusalia kwenye klabu baada ya mwisho wa msimu. (Telegraph)

Chanzo cha picha, Getty Images
Paris-St Germain wanammezea mate beki wa Juventus mwenye miaka 27 Mbrazil Alex Sandro, ambaye awali amehusishwa na Manchester United. (Le10 Sport - in French)
West Ham wako kwenye hatari ya kumpoteza mlinzi wa miaka 19 raia wa Ireland Declan Rice baada ya kukataa nyongeza ya mshahara wa pauni 12,000 kwa wiki. (Mail)

Chanzo cha picha, Getty Images
Arsenal, Manchester United, Liverpool, Chelsea na Newcastle ni kati ya vilabu 18 ambavyo vimewatuma maajenti kumtazama kipa wa Benfica Mjerumani Odisseas Vlachodimos, 24. (Record - in Portuguese)
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho alimlaumu kiungo wa kati Paul Pogba, 25, kwa bao lilifungwa na Wolves huko Old Trafford siku ya Jumamosi. (Sun)

Chanzo cha picha, Getty Images
Meneja wa zamani wa England Sven-Goran Eriksson yuko njiani kukiongoza klabu ya Iran ya Tractor Sazi, kilichomfuta kocha wa Wales na Real Madrid John Toshack mapema mwezi huu. (Sun)
Aston Villa wako tayari kuanza mazungumzo na mlinzi wa Wales James Chester, 23, kuhusu mkataba mpya. (Telegraph)

Chanzo cha picha, Getty Images
Bayern Munich wanammezea mate mlinzi mwenye miaka 22 wa RB Leipzig mjerumani Lukas Klostermann. (Sport Mediaset - in Italian)
Mtoto wa Meneja wa Cletic Brendan Rogers, Anton atashinda mkataba na klabu yenye matattizo ya Falkirk kufuatia majaribio. Kiungo huyo wa katu wa Northen Ireland alicheza dhidi ya St Mirren reserves wiki iliyopita na Dundee United siku ya Jumatau. (Falkirk Herald)
Bora zaidi kutoka Jumatatu
Mlinzi wa Manchester United Chris Smalling anataka kusaini mkataba mpya huko Old Trafford. Mchezaji huyo wa kimataifa mwenye miaka 28 wa England ana chini ya miezi 12 iliyobaki mkataba wake wa sasa kukamilika. (Star)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiungo wa kati wa Borussia Dortmund Mjerumani Mario Gotze, 26, ameshuriwa kujiunga na meneja wake wa zamaniaJurgen Klopp huko Liverpool. (Sky Sports)
David Beckham anafanya mazungumzo na mchezaji mwenzake wa zamania huko Real Madrid Zinedine Zidane kuhusu kukisimamia klabu yake ya Inter Miami katika ligi ya MLS. (Mirror)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kiungo wa kati wa Chelsea na Ubelgiji Eden Hazard, 27, anasema anahisi kuwa katika hali nzuri asilimia 200 licha ya kupumzishwa na meneja Maurizio Sarri kati kati ya wiki. Alirudi uwanjani akiwa kikosi cha kwanza wakati wa mechi iliyomalizika kwa sare siku ya Jumapili na West Ham. (Sky Sports)

Chanzo cha picha, Getty Images
Kipa mwenye miaka 25 wa Besiktas Loris Karius -ambaye yuko kwa mkopo huko Liverpool anasema anapata motisha kutoka kwa kipa wa zamani wa Ujerumani Olivier Kahn. (Bild - in German)
Wachezaji wa Everton wanaamini wanafanya maandalizi mengi wanapojiandaa kwa mechi za Ligi ya Primia chini ya usimamizi wake Marco Silva. (Sun)












