Tetesi za soka Ulaya Jumamosi 20.07.2018: Chelsea, Barcelona, Real Madrid ,Man United, Thibaut Courtois, Marcos Rojo, Willian na Hazard

Winga wa Chelsea na Brazil Willian, 29, anatarajiwa kujiunga na Manchester United kwa dau la £66m huku klabu hiyo ya Old Trafford pia ikiwa na hamu ya kutaka kumsajili beki wa The Blues mwenye umri wa miaka 32 Gary Cahill. (Express via Tuttosport)
Chelsea imemuorodhesha Kipa wa Uingereza Jordan Pickford, 24, kuwa lengo lao kuu iwapo kipa wake Thibaut Courtois, 26, ataondoka na kuelekea Real Madrid msimu huu (Sky Sports)
Manchester United italazimika kuilipa Leicester dau la rekodi ya £80m kwa Leicester ili kuweza kumleta beki wa Uingereza Harry Maguire , 25, Old Trafford. (Star)
Leicester City inafikiria kuwasilisha ombi la £35m kwa beki wa Newcastle, 24 Jamaal Lascelles, hatua ambayo itamfungulia njia Harry Maguire kuelekea Old Trafford. (Sun)

Manchester United itamuuza Marcos Rojo na Matteo Darmian, 28 ili kupata fedha za kumnunua Maguire. (Mirror)
Wolves inamlenga raia wa Argentine Rojo, 28, huku mkufunzi wa Manchester United Jose Mourinho akianza kuwajaribu mabeki tofauti. (Independent)
Maurizio Sarri yuko tayari kumpatia Eden Hazard cheo cha kuwa nahodha wa Chelsea katika jaribio la kumzuia mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27 kuondoka katika klabu hiyo. (Express)
Chelsea itaendelea kusisitiza dau la kuvunja rekodi la £200m kwa Real Madrid kumnunua Hazard. (Mail)
Crystal Palace inafikiria kumsaini mshambuliaji Danny Ings lakini italazimika kuafikia dau linalohitajika na Liverpool la thamani ya £20m ili kumnunua mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Guardian)

Chanzo cha picha, Getty Images
Leicester City, Newcastle United na Southampton pia wamewasilisha maombi ya kutaka kumsajili mshambuliaji huyo wa Liverpool Ings. (Times - subscription required)
Beki wa Juventus Daniele Rugani amekubali uhamisho wa kuelekea Chelsea lakini ajenti wa mchezaji huyo wa Itali ,23, anasema kuwa klabu hiyo ya Serie A haina haja ya kumuuza. . (London Evening Standard)
Crystal Palace bado ina hamu ya ya kumsaini kungo wa kati wa Senegal Cheikhou Kouyate, 28, huku West Ham ikisubiri maombi ya hadi dau la £10m kwa mchezaji huyo kuuzwa. (Sky Sports)
Chelsea inafikiria kumzuia mshambuliaji wake Alvaro Morata, 25, msimu huu na bado inataka kuwasilisha ombi la kumnunua Gonzalo Higuain, 30 kutoka Juventus. (London Evening Standard)

Besiktas iko katika mazungumzo na Liverpool kuhusu usajili wa kipa wa Ubelgiji Simon Mignolet, 30, huku kiungo wa kati wa Serbia Lazar Markovic, 24, akitarajiwa kuondoka Anfield baada ya kunyatiwa na klabu ya Ugiriki ya Olympiakos. (Mail)
Beki wa kulia wa Arsenal na Uhispania ,23, Hector Bellerin anasema kuwa itakuwa wazimu kuzungumza kuhusu kuondoka katika klabu hiyo licha ya kuhusishwa na uhamisho wa kuelekea Barcelona na Manchester City. (London Evening Standard)
Manchester United imemwambia beki wa Ivory Coast Eric Bailly, 24, kwamba hauzwi. (Manchester Evening News)

Mkufunzi wa Stoke Gary Rowett amepinga uvumi unaomuhusisha kipa wa Uingereza Jack Butland, 25, anayedaiwa kutaka kuelekea Chelsea. (Star)
Winga wa Crystal Palace Wilfried Zaha, 25, alichapisha ujumbe usioeleweka katika mtandao wa kijamii na kuzua hisia kuhusu hatma yake , huku Everton na Borussia Dortmund zikimnyatia winga huyo mwenye thamani ya £60m . (Mail)
Klabu ya Chelsea ina hamu ya kumsajili Zaha, na inamtaka mchezaji huyo kabla ya kufungwa kwa dirisha la uhamisho . (Star)
Aston Villa inafikiria kumsaini kipa wa Ureno,22, Andre Moreira kutoka klabu ya Atletico Madrid, (Sun)

Chanzo cha picha, Getty Images
Barcelona itafanya mazungumzo na West ham wikendi hii kuhusu uwezekano wa kumsaini kinda wa The Hammers na Ureno Domingos Quina,18, kwa dau la £600,000 . (Sky Sports)
Mkufunzi wa Liverpool Jurgen Klopp amemshutumu beki wa Real Madrid Sergio Ramos kwa kuwa na tabia ya mwanamieleka katika ushindi wa Real Madrid wakati wa fainali ya kombe La vilabu bingwa Ulaya.(Guardian)
Tetesi za soka Ijumaa 27.07.2018
Manchester United bado ina matumaini kusaini mkataba na winga wa Milan Ivan Perisic mwenye umri wa miaka 29 na itamuuza tu mshambuliaji wa Ufaransa Anthony Martial, mwenye umri wa miaka 22, ikiwa mchezaji huyo wa Croatian atapatikana. (Mirror)

Chanzo cha picha, EPA
Mlinzi wa Tottenham raia wa Ubelgiji Toby Alderweireld, mwenye umri wa miaka 29, amesalia kuwa ndiye anayepewa kipaumbele kusaini mkataba na Manchester United lakini the Londoners wanataka £55m au Anthony Martial ajumuishwe katika mazungumzo ya mkataba. (Independent)

Mmiliki wa Spurs Daniel Levy anaamini kuwa anaweza kusaini mkataba na mchezaji wa safu ya kati wa Aston Villa Muingereza Jack Grealish, mwenye umri wa miaka 22, kwa £20m. (Mirror)
Liverpool hawana nia ya kusaini mkataba na mlinzi wa Besiktas Domagoj Vida, mwenye umri wa miaka 29,licha ya kuwa na uhusiano na timu ya taifa ya Croatia. (Liverpool Echo)
Chelsea imeiambia AC Milan ilipe hadi £62m ikiwa wanataka kusaini mkataba na mshambuliaji Muhispania Alvaro Morata mwenye umri wa miaka 25. (Sky Sports)

Maafisa wa Chelsea wamesafiri hadi Italia kusaini mkataba na mlinzi wa Juventus Daniele Rugani, mwenye umri wa miaka 23, lakini wanasitasita kutimiza kiwango cha thamani yake cha £40m (Times - subscription required)
Mmiliki wa Blues Roman Abramovich na mkurugenzi Marina Granovskaia watakutana mjini Nice kushauriana kuhusu malengo yao ya uhamisho wa wachezaji (Evening Standard)
Barcelona wako tayari kukubali pendekezo la Everton la kiwango cha £27m kumnunua mlinzi wa timu ya taifa ya Colombia Yerry Mina, mwenye umri wa miaka 23. (Goal)

Chanzo cha picha, Empics
Mchezaji wa Everton wa safu ya kati Muholanzi Davy Klaassen, mwenye umri wa miaka 25, anazungumza na Werder Bremen juu ya hatua ya kumnunua kwa zaidi ya £13m . (Liverpool Echo)
Crystal Palace na Everton wana azma ya kusaini mktaba na mchezaji wa kiungo cha kati wa Roma mwenye umri wa miaka 27 Mfaransa French Maxime Gonalons kwa £10m. (Evening Standard)
West Ham wanaangalia uwezekano wa kumchukua mchezaji wa zamani wa kiungo cha kati wa Paris Saint-Germain Mfaransa Hatem Ben Arfa, mwenye umri wa miaka 31, kwa bila malipo. (Foot365 via Sports Mole)
Mchezaji wa safi ya mashambulizi wa Arsenal na Ufaransa Thierry Henry anachunguzwa kwa ajili ya fursa ya kuchukua nafasi ya meneja baada ya Aston Villa kuamua kusalia na Steve Bruce kama mkuu wake. (Mirror)

Chanzo cha picha, EPA
Brighton wanakaribia kusaini mkataba na mchezaji wa safu ya mashambulizi raia wa Ecuador Billy Arce mwenye umri wa miaka 20 kutoka timu ya Independiente del Valle. (Diario Expreso via Sport Witness)
Fenerbahce inataka kumchukua mlinzi wa Stoke Muholanzi Bruno Martins Indi, mwenye umri wa miaka 26, kwa mkataba wa deni la msimu. (Takvim - in Turkish)

Derby wako tayari kumuuza Mshambuliaji wa Czech Matej Vydra, mwenye umri wa miaka 26, kwa Leedskatika mkataba wa £11m, na watatumia pesa kumnunua mshambuliaji wa Ipswich Muingereza Martyn Waghorn mwenye umri wa miaka 28 (Sun)
Blackburn watasaini mkataba na mchezaji wa safu ya kati wa Chelsea Muingereza Kasey Palmer, akiwa na umri wa 21, kwa deni hadi mwishoni mwa mwaka huu . (Sky Sports)
Rangers wataangalia uwezekano wa kusaini mkataba na mchezaji wa safu ya kati Muingereza Kean Bryan, mwenye umri wa miaka 21 anayechezea Manchester City , ikiwa mchezaji wa safu ya kati wa Uingereza Josh Windass, mwenye umri wa miaka 24, ataondoka Ibrox. (Mail)












