Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Messi kusalia Barcelona hadi 2021
Mshambuliaji nyota wa klabu ya Barcelona Lionel Messi amekubali kutia saini mkataba mpya ambao utamuweka katika klabu hiyo hadi 2021.
Messi, 30, alijiunga na klabu ya Barca akiwa na miaka 13.
Mchezaji huyo anatarajiwa kutia saini mkataba huo atakaporejea kushiriki mazoezi.
Messi alifunga ndoa mwishoni mwa wiki mjini Rosario, Argentina.