Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kyrgios aing'arisha Australia Davies Cup
Nick Kyrgios ameiongoza vyema timu yake ya Australia kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Davies Cup baada ya kufanikiwa kuichapa Marekani.
Wameshinda kwa seti 7-6 (7-4) 6-3 6-4.
Australia iliyokuwa ikiongozwa na Lleyton Hewitt kwa sasa watavaana na timu ya Ubelgiji katika hatua hiyo ya nusu fainali baada ya kuwachapa Italia siku ya jana Jumapili.
Washindi mara tano wa michuano hiyo Uhispania walitolewa kirahisi na Serbia baada ya kurejea kwa mchezaji mahiri Novak Djokovic katika kikosi hicho.
Kwa upande wa Uingereza walishindwa kuendelea na mihuano hiyo baada ya kuchapwa na Ufaransa siku ya Jumapili.