Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
WADA: Urusi haijabadilika kimichezo
Rais wa shirikisho la kimatifa la kupambana na dawa za kusisimua misuli WADA, amesema kuwa bado michezo ya nchini Urusi haijashawishi Dunia kuwa imebadilika.
Akiongea katika mkutano wa WADA mjini Glasgow Craig Reedie amesema wakati kunafanyika maendeleo baadhi ya miji ya Urusi bado imefungiwa na wachunguzi kutoka shirika hilo.
Mkuu mpya wa kupambana na dawa za kusisimua misuli nchini Urusi Vitaly Smirnov amekanusha kuwa walitetea mfumo wa kutumia dawa za kusisimua misuli na kusema kuwa ni tatizo la Dunia nzima.
Wanariadha na watunisha misuli wa Urusi walipigwa marufuku kushiriki katika michezo ya Olimpiki ya mwaka huu mjini Rio De Jeneiro nchini Brazili.
Ripoti ya pili na ya Mwisho ya madai kutoka WADA inatarajiwa kutolewa mwezi ujao juu ya udaganyifu wa Urusi katika michezo.