Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Samir Nasri: Guardiola huwataka wachezaji kutofanya mapenzi baada ya saa 6 usiku
Mchezaji wa Ufaransa katika safu ya kati Samir Nasri amefichua kwamba mojawapo ya ufanisi mkubwa wa mkufunzi Pep Guradiola ni kuwaagiza wachezaji wake kutofanya mapenzi baada ya saa sita usiku.
Katika mahojiano na runinga ya Ufaransa,Nasri amesema kuwa Guardiola aliweka sheria hiyo hata iwapo kungekuwa hakuna mechi siku iliofuatia ili wachezaji wapate usingizi mwanana.
Hata Lionel Messi anayetambulika kuwa mchezaji bora duniani hakuwachwa nje wakati wa uongozi wa Guradiola katika timu ya Barcelona.
Nasri amesema kuwa hatua hiyo ilimwezesha Messi kutopata majeraha ya misuli