Trump kushinikiza mpango mpya wa amani katika mazungumzo na Netanyahu

Rais wa Marekani Donald Trump amesema atasukuma mpango mpya wa amani wa kumaliza vita vya Israel na Gaza wakati wa mazungumzo ya White House na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu.

Muhtasari

Moja kwa moja

Na Asha Juma

  1. Trump kuipatia Ukraine makombora ya masafa marefu, Vance asema

    Watu kadhaa waliuawa katika shambulio la saa 12 mjini Kyiv siku ya Jumapili huku zaidi ya 70 wakijeruhiwa katika eneo lote la Ukraine.

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Marekani inazingatia ombi la Ukraine la kutaka makombora ya masafa marefu ya Tomahawk, Makamu wa Rais wa Marekani JD Vance amesema.

    Hatahivyo, Vance aliongeza kuwa Rais Donald Trump atakuwa akifanya "uamuzi wa mwisho" kuhusu suala hilo.

    Kwa muda mrefu Kyiv imekuwa ikitoa wito kwa washirika wake wa Magharibi kuipatia silaha zinazoweza kugonga miji mikubwa ya Urusi iliyo mbali na mstari wa mbele, ikisema kwamba zingeisaidia Ukraine kudhoofisha kijeshi Urusi na kumaliza vita.

    "Ikiwa gharama ya kuendeleza vita vya Moscow ni kubwa mno, italazimika kuanzisha mazungumzo ya amani," naibu waziri wa ulinzi Ivan Havryliuk aliambia BBC.

    Msemaji wa Kremlin Dmitry Peskov alipuuza kauli ya Vance, akisema "hakuna dawa ambayo inaweza kubadilisha hali ya serikali ya Kyiv." "Iwe ni Tomahawks au makombora mengine, hayataweza kubadilisha nguvu," aliongeza.

    Makombora ya Tomahawk yana masafa ya kilomita 2,500 (maili 1,550), ambayo yataifanya Moscow kufikia Ukraine. Wakati Vance alisalia kuwa na utata kuhusu ombi la Ukraine kwa Tomahawks katika hotuba yake siku ya Jumapili, mjumbe maalum wa Marekani nchini Ukraine, Keith Kellogg, alieleza Trump alikuwa tayari ameidhinisha mashambulizi ndani ya ardhi ya Urusi.

    Alipoulizwa kwenye Fox News kama Washington iliruhusu Kyiv kufanya shambulizi la masafa marefu ndani ya Urusi katika matukio maalum, Kellogg alisema: "Jibu ni ndiyo, tumia uwezo wa kupiga kwa kina, hakuna vitu kama mahali patakatifu."

    Maoni ya Vance na Kellogg yanalingana na mabadiliko ya hivi karibuni ya utawala wa Marekani kuhusiana na vita.

    Siku ya Jumapili, shambulizi kubwa la saa 12 lililohusisha mamia ya ndege zisizo na rubani na karibu makombora 50 lilisababisha vifo vya watu wanne mjini Kyiv na takribani 70 kujeruhiwa.

    Mwanahabari wa Ukraine Havryliuk aliiambia BBC kwamba Urusi itaongeza tu ukubwa na ukali wa mashambulizi yake ya angani.

    Unaweza kusoma;

  2. Mahakama ya Sudan Kusini yakataa ombi la Makamu wa Rais wa zamani la kusitisha kesi ya mauaji na uhaini

    Riek Machar amekuwa chini ya kizuizi cha nyumbani tangu Machi

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Mahakama maalum nchini Sudan Kusini imesema kuwa ina mamlaka ya kuwafungulia mashtaka Makamu wa Rais aliyesimamishwa Riek Machar na washtakiwa wenzake saba, wanaoshtakiwa kwa mauaji, uhaini na uhalifu dhidi ya binadamu.

    Mahakama ilitupilia mbali mapingamizi yote ya timu ya wanasheria wa Machar kuhusu mamlaka yake, uhalali wa kesi hiyo, na madai kwamba alikuwa na kinga dhidi ya kushtakiwa.

    Kesi hiyo itaendelea Jumatano. Machar ametupilia mbali mashtaka yaliyoletwa dhidi yake wiki mbili zilizopita.

    Wameibua hofu ya kurudi kwenye vita vya wenyewe kwa wenyewe.

    Mashtaka hayo yanatokana na shambulio la mwezi Machi lililofanywa na wanamgambo wanaodaiwa kuwa na uhusiano na Machar, na kusababisha vifo vya wanajeshi 250 na jenerali mmoja.

    Tangu wakati huo, amekuwa chini ya kizuizi cha nyumbani.

    Timu ya mawakili ya Machar ilidai kuwa makosa hayo ya uhalifu yasihukumiwe na mahakama ya kitaifa bali mahakama ya mseto chini ya Umoja wa Afrika, kwa mujibu wa Mkataba wa Amani wa 2018 uliomaliza vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyodumu kwa miaka mitano kati ya vikosi vyake na wale watiifu kwa Rais Salva Kiir.

    Unaweza kusoma;

  3. Trump kushinikiza mpango mpya wa amani katika mazungumzo na Netanyahu

    Itakuwa ni ziara ya nne kwa Netanyahu katika Ikulu ya White House tangu Trump arudi ofisini Januari

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Marekani Donald Trump amesema atasukuma mpango mpya wa amani wa kumaliza vita vya Israel na Gaza wakati wa mazungumzo ya White House na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu siku ya Jumatatu.

    Trump amezungumza kuhusu matarajio ya kufikia makubaliano, akiwaambia waandishi wa habari siku ya Ijumaa: "Nadhani tuna makubaliano".

    Lakini Netanyahu alisema Jumapili "bado haijakamilika", wakati Hamas walisema hawajatuma pendekezo hilo rasmi.

    Kwa mujibu wa nakala zilizovuja za mpango huo zilizochapishwa na vyombo vya habari vya Marekani na Israel, kuachiliwa kwa mateka wote ndani ya saa 48 baada ya mkataba huo kumethibitishwa.

    Mara watakaporudishwa, Israel itawaachia huru mamia ya wafungwa wa Kipalestina wanaotumikia kifungo cha maisha.

    Wanachama wa Hamas wanaojitolea kuleta amani watapewa msamaha na kupita salama kutoka Gaza na kundi hilo halitakuwa na jukumu la baadaye katika eneo hilo.

    Miundo mbinu yote ya kijeshi ya Hamas itaharibiwa. Jeshi la Israel la Ulinzi (IDF) litaondoka hatua kwa hatua kutoka Ukanda wa Gaza na kutawaliwa na serikali ya mpito.

    Unaweza kusoma;

  4. China yawahukumu kifo watu 11 wa familia moja

    .

    Chanzo cha picha, CCTV

    Mahakama ya China imewahukumu kifo watu 11 wa familia yenye sifa mbaya iliyokuwa ikiendesha vituo vya utapeli nchini Myanmar, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya serikali ya China.

    Makumi ya jamaa wa familia ya Ming walipatikana na hatia ya kufanya vitendo vya uhalifu, huku wengi wakipokea vifungo vya muda mrefu gerezani.

    Familia ya Ming ilifanya kazi katika moja ya koo nne zilizoendesha mji wa Laukkai, karibu na mpaka wa Myanmar, na kuugeuza kuwa kitovu cha kamari, dawa za kulevya na vituo vya utapeli.

    Hatimaye Myanmar ilichukua hatua na kuwakamata watu wengi wa familia hizo mwaka wa 2023 na kuwakabidhi kwa mamlaka ya China.

    Jumla ya wanafamilia 39 wa Ming walihukumiwa siku ya Jumatatu katika mji wa mashariki wa Wenzhou, kulingana na ripoti ya shirika la utangazaji la serikali ya China CCTV.

  5. Denmark yapiga marufuku droni za kibinafsi kabla ya kongamano la EU

    R

    Chanzo cha picha, EPA

    Denmark imepiga marufuku ndege zote zisizo na rubani wiki hii kabla ya kongamano la Umoja wa Ulaya ambalo litafanyika njini Copenhagen, waziri wa uchukuzi wa nchi hiyo alitangaza Jumapili.

    Wazara hiyo ilisema hatua hitua hiyo ilifikiwa ili "kurahisisha shughuli za usalama" kwa polisi, na kwamba hawataruhusu "droni za kigeni kuibua hali ya taharuki".

    Denmark ni mojawapo wa mataifa kadhaa za Ulaya zilizoripoti "visa vya droni kuingia anga zao bila idhini" katika wiki za hivi karibuni, tukio la hivi punde likiwa la moja ya droni hizo zikipaa juu ya kambi yake ya kijeshi ya siku ya Jumamosi.

    Mawaziri wa ulinzi kutoka nchi 10 za Umoja wa Ulaya wamekubali kuunda "ukuta wa ulinzi wa ndege zisizo na rubani" ili kukabiliana na matukio hayo, na Nato inasema "imeimarisha ulinzi" katika eneo lote la Baltic.

    Marufuku hiyo itadumishwa hadi tarehe 3 Oktoba, na yule atakayekiuka atakabiliwa na faini au kifungo cha hadi miaka miwili.

    Pia unaweza kusoma:

  6. Ushelisheli kuandaa duru ya pili ya uchaguzi wa urais

    Duru ya pili itafanyika kuanzia tarehe 9-11 Oktoba

    Chanzo cha picha, AFP via Getty Images

    Maelezo ya picha, Duru ya pili itafanyika kuanzia tarehe 9-11 Oktoba

    Ushelisheli inatarajiwa kufanya marudio ya uchaguzi wake wa urais kati ya wagombea wawili wakuu, baada ya kukosekana kwa mshindi wa moja kwa moja.

    Kiongozi wa upinzani Patrick Herminie alipata 48.8% ya kura dhidi ya Rais aliyeko madarakani Wavel Ramkalawan ambaye alipata 46.4%, tume ya uchaguzi ilitangaza.

    Kulingana na kanuni za uchaguzi, mgombea lazima apate zaidi ya 50% ya kura ili kutangazwa mshindi.

    Duru ya pili ya uchaguzi huo sasa umeratibiwa kufanyika wiki ijayo.

    Ushelisheli ni nchi ndogo zaidi barani Afrika katika Bahari ya Hindi na idadi ya zaidi ya watu 120,000.

    Wagombea wanane waliwania urais katika uchaguzi uliofanyika wa wiki iliyopita.

  7. Chama kinachounga mkono EU chapata ushindi mkubwa katika uchaguzi licha ya madai ya kuingiliwa na Urusi

    .

    Chanzo cha picha, Anadolu via Getty Images

    Chama kinachounga mkono Ulaya cha Rais wa Moldova Maia Sandu kimepata ushindi mkubwa wa ubunge katika uchaguzi unaoonekana kuwa muhimu kwa mustakabali wa nchi yake kuelekea EU.

    Sandu alikuwa ameonya kuhusu "uingiliaji mkubwa wa Urusi" baada ya kupiga kura, akisema mustakabali wa nchi yake, inayozungukwa na Ukraine na Romania, uko hatarini.

    Chama chake cha Action and Solidarity (PAS) tayari kilikuwa kimepata 50% ya kura, huku kura nyingi kati ya 1.6m zikiwa zimehesabiwa, kikiwa kifua mbele ya Muungano unaopendelea Urusi ulio chini ya 25%.

    Waliojitokeza walikuwa 52%, idadi ya juu kuliko miaka ya hivi karibuni.

    Mmoja wa viongozi wakuu wa upinzani, Igor Dodon, alikuwa amedai ushindi hata kabla ya matokeo na akaitisha maandamano nje ya bunge siku ya Jumatatu.

  8. Wakenya waliojikuta katika vita nchini Urusi waokolewa

    .

    Chanzo cha picha, EPA-EFE/REX/Shutterstock

    Serikali ya Kenya inasema ujumbe wake huko Urusi umeokoa na kuwarudisha raia watatu ambao walisafirishwa kwenda nchini humo.

    Hili linawadia wiki moja baada ya Wizara ya Mambo ya nje kusema ilikuwa inafuatilia ripoti za Wakenya kadhaa zinazodai walilazimishwa kuingia kwenye jeshi la Urusi na baadaye kutekwa kama wafungwa wa vita huko Ukraine.

    Katika taarifa kwenye vyombo vya habari vya kijamii, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya nje nchini Kenya Korir Sing'oei alisema wanaume wawili na mwanamke mmoja wako salama na wanarudi nyumbani kwa familia zao.

    Tangazo hilo linafuatia operesheni ya usalama jijini Nairobi mwishoni mwa wiki iliyopita ambapo viongozi waligundua kile wanachoamini kuwa ni kikundi cha usafirishaji watu kilichowashawishi raia na ahadi za kazi zenye faida kubwa huko Moscow lakini baada ya kuwasili wakajikuta wamelazimishwa kuingia katika jeshi la Urusi na kupelekwa mstari wa mbele katika vita dhidi ya Ukraine.

    Kesi hiyo imevutia nadhari baada ya jeshi la Ukraine kutoa video ya mwanariadha wa Kenya, ambaye alisema alidanganywa kujiunga na jeshi la Urusi na aliomba kurudishwa nyumbani.

    Pia unaweza kuoma:

  9. Tazama: China yafungua daraja kubwa zaidi duniani

    Maelezo ya video, Tazama: China yafungua daraja kubwa zaidi duniani

    China imefungua rasmi daraja kubwa zaidi duniani kwa umma.

    Daraja la Grand Canyon la Huajiang lina urefu wa 625m (2,083ft) juu ya bonde katika mkoa wa Guizhou.

    Wenye mamlaka wanasema daraja hilo linapunguza muda wa kusafiri kati ya pande mbili za bonde hilo kutoka saa mbili hadi dakika mbili.

    Mapema mwaka huu mnamo mwezi Agosti, timu husika ilifanya majaribio kwa kuendesha malori 96 kwenye sehemu zilizotengwa ili kuangalia uadilifu wa muundo wa daraja.

    Daraja hilo sasa limeweka rekodi ya daraja kubwa zaidi ulimwenguni lililojengwa katika eneo lenye mlima.

    Piaunaweza kusoma:

  10. Takriban watu wanne wafariki na wengine kujeruhiwa katika tukio la ufyatuaji risasi kanisani huko Michigan

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Takriban watu wanne wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa baada ya mtu mwenye silaha kuliendesha gari katika kanisa la Michigan, kufyatua risasi na kuchoma jengo hilo, polisi wanasema.

    Maafisa walisema shambulio dhidi ya Kanisa la Jesus Christ of Latter-day Saints huko Grand Blanc, mji ulio umbali wa maili 60 (kilomita 100) kaskazini magharibi mwa Detroit, lilitokea wakati wa ibada ya Jumapili iliyovutia mamia ya watu.

    Mshukiwa huyo aliyetambulika kwa jina la Thomas Jacob Sanford, 40, kutoka Burton, Michigan, baadaye aliuawa kwa kupigwa risasi na polisi katika eneo la kuegesha magari la kanisa.

    Mamlaka inachunguza tukio hilo kama "kitendo cha vurugu zilizolengwa", lakini wanasema nia bado haijafahamika.

  11. Boti ndogo yaweka rekodi ya kubeba wahamiaji wengi zaidi kwenye kivuko

    .

    Chanzo cha picha, Getty Images

    Boti ndogo ilivuka kivuko siku ya Jumamosi ikiwa imebeba wahamiaji 125, idadi kubwa zaidi kuwahi kusafari katika chombo kimoja cha aina hiyo.

    Rekodi hiyo imepita ile iliyowekwa mwezi Agosti wakati watu 106 walipojaribu kuvuka kwa kutumia boti moja.

    Takwimu kutoka Ofisi ya Mambo ya Ndani zinaonyesha wahamiaji 895 walivuka kivuko kwa boti 12 siku ya Jumamosi, wakati karibu watu 33,000 wamefanya hivyo tangu kuanza kwa 2025.

    Hili linatokea baada ya mhamiaji mwingine kufariki akijaribu kuvuka kivuko, na mwili kupatikana Jumapili asubuhi kwenye ufuo karibu na Boulogne-sur-Mer kaskazini mwa Ufaransa, kulingana na shirika la habari la AFP.

    Pia unaweza kusoma:

  12. Raia wa Marekani aachiliwa na Taliban baada ya kuzuiliwa kwa miezi tisa

    .

    Chanzo cha picha, Qatari Diplomat via Reuters

    Raia wa Marekani aliyeshikiliwa na kundi la Taliban nchini Afghanistan kwa muda wa miezi tisa ameachiliwa huru kufuatia mazungumzo yaliyoongozwa na wapatanishi wa Qatar, maafisa wanasema.

    Mwanamume huyo aliyetambulika kwa jina la Amir Amiry, ni Mmarekani wa tano kuachiliwa kutoka kizuizini nchini Afghanistan mwaka huu. Alikuwa njiani kurejea Marekani siku ya Jumapili.

    Waziri wa mambo ya nje wa Marekani Marco Rubio aliishukuru Qatar kwa "juhudi zake za kidiplomasia zisizochoka", ambazo alisema ni muhimu katika kufanikisha kuachiliwa kwa Bw Amiry.

    Sababu ya kuzuiliwa kwa Bw Amiry bado haijafahamika. Rubio alisema kuwa "alizuiliwa kimakosa".

    Waziri huyo wa mambo ya nje ameongeza kuwa raia zaidi wa Marekani bado "wanazuiliwa kinyume cha sheria" nchini Afghanistan na kwamba utawala wa Trump ulikuwa ukifanya kazi ya kuwaachilia huru.

    Wizara ya mambo ya nje ya Qatar ilisema iliwezesha kuachiliwa kwa Bw Amiry na kwamba alikuwa njiani kuelekea Doha kabla ya kusafiri kwenda Marekani.

    Pia unaweza kusoma:

  13. Trump ana matumaini ya kufikiwa kwa mpango wa amani wa Gaza

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Rais wa Marekani Donald Trump anatarajia kukamilisha pendekezo la mpango wa amani wa Gaza katika mkutano wa Jumatatu na Waziri Mkuu wa Israel, Trump aliambia Reuters siku ya Jumapili, wakati vifaru vya Israel vikisonga mbele zaidi katika mji wa Gaza huku Hamas ikisema imepoteza mawasiliano na mateka wawili waliokuwa wameshikiliwa huko.

    Hatima ya mateka hao wawili, waliosababisha hisia kali ndani ya Israel, inaweza kuwa na athari mbaya kwenye mkutano kati ya Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu na Trump hii leo siku ya Jumatatu.

    Kikosi cha kijeshi cha Hamas, Al-Qassam Brigedi, kiliitaka Israel siku ya Jumapili kuwarudisha nyuma wanajeshi wake na kusitisha mashambulizi ya anga katika mji wa Gaza kwa saa 24 ili wapiganaji waweze kuwapata mateka.

    Trump aliliambia shirika la habari la Reuters katika mahojiano ya simu kuwa amepokea "jibu la kutia moyo" kutoka kwa Israel na viongozi wa Kiarabu kuhusu pendekezo la mpango wa amani wa Gaza na kwamba "kila mtu anataka makubaliano yafikiwe."

    Hamas ilisema bado haijapokea pendekezo lolote kutoka kwa Trump wala kutoka kwa wapatanishi.

    Israel imefanya shambulio kubwa la ardhini katika mji wa Gaza, na kusambaratisha wilaya nzima huku ikiamuru mamia kwa maelfu ya Wapalestina kukimbilia katika kambi zilizo na mahema, katika kile Netanyahu anasema ni kutaka kuangamiza Hamas.

    Soma zaidi:

  14. ‘Urusi haina nia ya kushambulia nchi za EU au NATO’ - Lavrov

    .

    Chanzo cha picha, Reuters

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Urusi Sergei Lavrov amesema nchi yake haina nia ya kushambulia nchi za Umoja wa Ulaya au wanachama wa NATO - lakini akaonya juu ya "kuchukua hatua madhubuti" kwa "uchokozi" wowote unaoelekezwa kwa Urusi.

    Katika hotuba ya kina iliyotolewa kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Jumamosi, Lavrov alisema kuwa vitisho vya nchi za Magharibi dhidi ya Urusi vinazidi kuwa "vya kawaida".

    Pia aliikosoa Israel, akisema kwamba wakati Urusi ililaani mashambulizi ya Hamas mnamo Oktoba 7, 2023, hakuna "uhalali" wa "mauaji ya kikatili" ya Wapalestina huko Gaza, au kwa mipango ya kunyakua Ukingo wa Magharibi.

    Awali Israel ilikuwa imesema kwamba operesheni yake huko Gaza ilikuwa muhimu ili kuwashinda Hamas.

    Takriban watu 65,926 wameuawa katika mashambulizi ya Israel, kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Gaza, huku takriban watu 1,200 wakiuawa na wengine 251 kuchukuliwa mateka katika mashambulizi ya Oktoba 7.

    Soma zaidi:

  15. Hujambo na karibu katika matangazo yetu mubashara. Tarehe ni 29/09/2029