Obama na Trump warushiana cheche za maneno

Rais wa Marekani Barack Obama amemshambulia vikali mgombea wa chama cha Republican Donald Trump akisema kwua hana uwezo kuwa rais.
Obama alitaka kujua ni kwa sababu gani chama cha Republiban kinaendelea kumuunga mkono bwana Trump.

Chanzo cha picha, Getty
Alisema kuwa kinyume na wagombea wengine wa zamani wa Republican, bawana Trump hana uwezo wa kushika wadhifa mkubwa zaidi duniani.
Trump alijibu kwa kumlaumu Obama kwa uongozi mbaya.








