Tetemeko la Ardhi Uturuki: Ulimwengu waungana baada kukumbwa na janga

Wakati Uturuki na Syria zikianza kutathmini uharibifu uliosababishwa na tetemeko la ardhi lenye kipimo cha 7.8 ambalo hadi sasa limesababisha vifo vya watu wasiopungua 4,800, nchi mbalimbali duniani zimejipanga kusaidia juhudi za uokoaji.

Mvua na theluji inaathiri waokoaji, lakini timu maalum kutoka mataifa mengi, ikiwa ni pamoja na Italia, Marekani, Israel na Taiwan - ziko njiani.

Picha zote zina haki miliki.