Amehudumu kwa mihula miwili kama gavana wa Lagos. 1999-2007
Amewakilisha Lagos magharibi katika bunge la seneti kuanzia 1992 hadi 1993.
Ni mwanasiasa mkongwe, hii ni mara ya kwanza kugombea urais.
Anapiga kampeni dhidi ya utawala wa kijeshi
Ameongeza pato la Lagos mara nne zaidi kutoka Naira bilioni 22.2 mwaka 1999 hadi Naira bilioni 220.9 mwaka 2007.
Akifanya kazi kama mkaguzi mkuu na baadaye mweka hazina wa Mobil Producing Nigeria, mojawapo ya nchi zinazozalisha mafuta kwa wingi.
Kukuza mauzo ya nje ya Nigeria na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje.
Kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira kwa vijana kwa nusu ndani ya miaka minne na kuunda nafasi za kazi milioni katika ICT ndani ya miaka miwili.
Kurekebisha mfumo wa haki ili kuzingatia kuzuia uhalifu na kuboresha imani kwa vikosi vya usalama.
Atiku Abubakar
Chama cha PDP
Umri, miaka 76
Makamu wa rais wa Nigeria kuanzia 1999-2007.
Ana Shahada ya Uzamili katika uhusiano wa kimataifa kutoka Chuo Kikuu cha Anglia Ruskin, Uingereza.
Afisa wa zamani wa forodha ambaye aliingia katika siasa mwanzoni mwa miaka ya 1980.
Amegombea mara tano urais ambapo hakufanikiwa, mnamo 1993, 2007, 2011, 2015 na 2019.
Ameanzisha Chuo Kikuu cha Marekani cha Nigeria, ambacho kilitoa ufadhili wa masomo kwa wasichana walioachiliwa wa Chibok.
Mfanyabiashara aliyefanikiwa na uwekezaji katika huduma za mafuta, kilimo, benki na sekta ya dawa.
Ubinafsishaji wenye utata wa ajenda ya mali ya serikali.
Kuipa sekta binafsi nafasi kubwa katika uchumi.
Kuimarisha umoja wa kitaifa kupitia usawa, haki ya kijamii miongoni mwa watu mbalimbali wa Nigeria.
Kurekebisha mfumo wa utawala wa Nigeria.
Peter Obi
Chama cha Wafanyakazi (LP)
Miaka 60
Gavana wa awamu mbili wa Jimbo la Anambra kutoka 2007 hadi 2014.
Alikua mgombea mwenza wa urais wakati wa uchaguzi wa mwaka 2019
Mfanyabiashara, alisoma falsafa katika Chuo Kikuu cha Nigeria, Nsukka.
Alianzisha hazina ya utajiri wa serikali ndogo yenye thamani ya takriban $156milioni katika bondi za thamani ya dola kufikia mwisho wa kipindi chake kama gavana.
Kasogeza Anambra kutoka nafasi ya 26 hadi ya 1 katika orodha ya majimbo yaliyofanya vyema katika mitihani ya kitaifa ya NECO na WAEC.
Kumiliki msururu wa biashara ya rejareja ambayo imeunda maelfu ya ajira.
Kuhakikisha uwajibikaji katika utawala na kupambana na rushwa.
Hamisha Nigeria kutoka kwa matumizi hadi uzalishaji.
Kutanguliza Maendeleo ya Mtaji wa Binadamu kupitia uwekezaji thabiti katika elimu ya STEM, afya, na maendeleo ya miundombinu.
Rabiu Kwankwaso
Chama cha NNPP
Miaka 66
Waziri wa ulinzi kuanzia 2002 hadi 2007.
Gavana wa Jimbo la Kano kutoka 1999 hadi 2003, na 2011 hadi 2015.
Aliwakilisha Eneo bunge la Shirikisho la Madobi katika Baraza la Wawakilishi mwaka wa 1992 na Wilaya ya Seneta ya Kano ya Kati kati ya 2015 na 2019.
Ana PhD Katika uhandisi wa umma kutoka Chuo Kikuu cha Sharda, India.
Juhudi za ufadhili na ufadhili wa masomo.
Aliongeza idadi ya walioandikishwa katika shule za msingi kutoka milioni moja mwaka 2011 hadi zaidi ya milioni tatu mwaka 2015 alipoondoka madarakani.
Kuanzisha chakula cha bure shuleni na sare kwa wanafunzi wa shule za msingi.
Kuanzisha Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Kano huko Wudil na Chuo Kikuu cha Kaskazini-Magharibi, vyuo vikuu vya kwanza na vya pili vya jimbo la Kano.
Kujenga ajira kupitia uwekezaji katika kilimo.
Kushughulikia ukosefu wa usalama.
Kuheshimu utawala wa sheria na kufuata taratibu zinazostahili.
Kuongeza mauzo nje na kupunguza utegemezi wa bidhaa kutoka nje
Kupunguza nusu ya ukosefu wa ajira kwa vijana ndani ya miaka minne
Kuchukua hatua kuhakikisha uhuru wa mahakama
Uchumi
Kusaidia uzalishaji motisha ya kodi
Kudhibiti bei za bidhaa za msingi ili kudhibiti mfumuko wa bei
Kuongeza uzalishaji wa gesi kwa 20%
Ajira
Kuunda ajira mpya milioni moja za ICT ndani ya miaka miwili
Kupunguza ukosefu wa ajira kwa vijana kwa kuhimiza benki za Biashara kutoa mikopo nafuu kwa biashara zinazoongozwa na vijana
Kusaidia wafanyabiashara na wataalamu milioni mbili katika kuwashauri vijana kutafuta kazi na kuanzisha biashara
Afya
Kuanzisha bima ya afya ya lazima ili kufidia angalau 40% ya watu ndani ya miaka miwili
Kuongeza idadi na ujuzi wa wafanyakazi wa afya, hasa wale walio katika huduma ya msingi
Kurudisha ujenzi wa kliniki zinazohamishika ili kuhakikisha kila mtu anaishi karibu na kituo cha afya cha msingi
Kuhimiza utengenezaji wa ndani wa dawa na chanjo muhimu
Usalama
Kuboresha mishahara na ustawi wa wafanyakazi wa usalama na kuanzisha fungu maalum kwa watu waliojeruhiwa na waliokufa
Kuboresha silaha, mifumo ya mawasiliano na usafiri wa vitengo vya kijeshi
Kuajiri, kutoa mafunzo na kuandaa vizuri zaidi wanajeshi wa ziada, polisi, wanajeshi na maafisa ujasusi
Kuondoa mashambulizi kwenye miundombinu muhimu ya kitaifa
Elimu
Kutengeneza viwango vipya vya ithibati kwa taasisi zote za masomo, kuanzia ngazi ya msingi hadi elimu ya juu
Kuanzisha utaratibu wa majaribio wa mkopo wa wanafunzi
Kuanzisha mfuko wa elimu maalum unaojumuisha mikopo isiyo na riba
Rushwa
Kiwango cha matumizi katika mishahara ya viongozi waliochaguliwa na watumishi wa umma
Kupunguza kiwango cha fedha kinachovuja kutoka kwa fedha za serikali
Kuwatuza wenye bidii ya kazi na kuwaondoa wafanyakazi hewa na miradi isiyo ya kawaida
Kupunguza urasimu wa utumishi wa umma na kupunguza ubadhirifu
Chama cha Labour
Vipaumbele vya juu
Kufanya mageuzi ya kuimarisha utawala wa sheria, kupambana vikali na rushwa na kupunguza gharama za utawala.
Kuitoa Nigeria kutoka kwenye uchumi wa matumizi hadi uchumi wa uzalishaji
Kuongeza tija ya watu binafsi kupitia uwekezaji katika maeneo kama vile sayansi, teknolojia na elimu
Uchumi
Kubadilisha uchumi kupitia mapinduzi ya kilimo na ukuaji wa viwanda unaozingatia mauzo ya nje
Kupunguza mfumuko wa bei kwa tarakimu moja, kuhakikisha uhuru wa benki kuu
Punguza utegemezi wa mauzo ya mafuta nje ya nchi
Ondoa vikwazo vya uingizaji wa fedha za kigeni na kuunda soko moja la fedha za kigeni
Ajira
Kuboresha upatikanaji wa fedha kwa biashara za kati na ndogo, vijana na wanawake, ili kusaidia kupunguza ukosefu wa ajira
Kuwekeza katika maendeleo ya mtaji wa watu
Kuboresha urahisi wa kufanya biashara ili kuvutia uwekezaji wa kigeni ili kuanza ukuaji wa viwanda
Kuunda mazingira ya biashara ambayo yatasaidia wanaoanza kustawi
Afya
Kuboresha mishahara na masharti ya huduma kwa wafanyakazi wa afya
Kutoa bima ya afya kwa Wanaigeria milioni 133 maskini zaidi
Kuboresha na kuendeleza utaalamu miongoni mwa wafanyakazi wa afya
Kutoa ufikiaji wa huduma za afya kwa bei nafuu na bora
Usalama
Komesha ujambazi na uasi kwa kuongeza imani kwa vikosi vya usalama na kujenga idara za usalama
Kuanzisha ushirikiano na nchi jirani ili kulinda mipaka
Kutengeneza sheria ya kuanzisha polisi jamii
Kuongeza idadi katika vikosi vya jeshi, polisi na mashirika mengine ya usalama na kuandaa ipasavyo mafunzo na fedha zao
Elimu
Kuwekeza katika mafunzo ya ufundi na ufundi stadi, michezo, ujasiriamali pamoja na uwekaji misimbo na ujuzi wa kidijitali kwa wanafunzi wa shule
Kuimarisha uwekezaji katika afya, elimu na makazi ili kuhakikisha kuwa hakuna mtoto anayeachwa nyuma
Kuruhusu mashirika ya binafsi kusimamia shule huku serikali ikidumisha usimamizi wa mtaala
Kutumia 14% ya bajeti ya serikali kwenye elimu
Rushwa
Kuzingatia sheria za uwajibikaji wa kifedha ambazo zinapaswa kuhakikisha usimamizi wa kifedha wa busara
Kuifanya mihimili yote ya serikali ifanyiwe ukaguzi wa kawaida
Kumaliza utaratibu wa ruzuku ya mafuta
Kuwa muwazi na kuwajibika katika shughuli za serikali
New Nigeria People's Party
Vipaumbele vya juu
Kutengeneza ajira kupitia uwekezaji katika kilimo
Kushughulikia ukosefu wa usalama
Kuheshimu utawala wa sheria na kufuata taratibu zinazostahili
Uchumi
Kupambana na rushwa serikalini ili kuongeza mapato
Kurekebisha soko la mitaji ili kulifanya liwe na ushindani na ufanisi kama chanzo cha fedha za biashara za muda mrefu
Kufanya usimamizi unaotegemewa, unaoaminika na ulio wazi wa kiwango cha ubadilishaji fedha
Ajira
Kupunguza kiwango cha ukosefu wa ajira hadi tarakimu moja
Kuhimiza vijana kuzingatia taaluma katika kilimo
Kuhimiza uwekezaji wa sekta binafsi katika viwanda vya kusindika chakula ili kutengeneza ajira kwa vijana
Afya
Marekebisho ya Mpango wa Taifa wa Bima ya Afya
Kupunguza utalii wa afya kupitia uboreshaji wa vituo vya afya, uboreshaji wa huduma, mafunzo ya wahudumu wa afya na uhamishaji na ununuzi wa teknolojia.
Kuongeza mgao wa bajeti kwa sekta ya afya
Usalama
Kuongeza rasilimali kwenye idara za kijasusi ili kukabiliana na ukosefu wa usalama
Kukuza uwiano na maridhiano ya kitaifa
Kuwa wazi zaidi kwa umma
Elimu
Kutoa fedha za kutosha kwa sekta ya elimu
Kuboresha taasisi zote za elimu ya juu zilizopo kabla ya kuunda mpya
Kuunga mkono juhudi za kujenga malazi kwa zaidi ya watoto milioni 20 wasiokwenda shule wanaoishi mitaani kwa sasa
Rushwa
Kurekebisha na kuimarisha taasisi za kupambana na rushwa
Kuendesha serikali ya uwazi na wazi
Kutumia teknolojia kuzuia rushwa
People's Democratic Party
Vipaumbele vya juu
Kuipa sekta binafsi nafasi kubwa katika uchumi
Kukuza umoja wa kitaifa kupitia uteuzi tofauti wa serikali unaozingatia usawa wa kikanda
Kurekebisha mfumo wa utawala wa Nigeria
Uchumi
Pato la Taifa mara mbili kwa kila mtu hadi $5,000 (£4,200) kufikia 2030
Kukuza uwekezaji wa miundombinu kwa lengo la kukuza haraka sehemu yake ya Pato la Taifa
Kuongeza uwezo wa kusafisha mafuta hadi mapipa milioni mbili kwa siku ifikapo 2027
Ajira
Kuunda nafasi mpya za kazi milioni tatu na kuondoa umaskini kwa watu milioni 10 kila mwaka
Kuanzisha programu ya kitaifa ya kutengeneza ajira kwa ufanisi zaidi, yenye gharama nafuu na endelevu
Kuunda vituo vya kuwasaidia wajasiriamali na vitovu vya kibiashara ili kusaidia biashara ndogo na za kati
Afya
Kuharakisha hatua kuelekea upatikanaji wa huduma za afya kwa bei nafuu na bora ifikapo 2030
Kuwapa motisha madaktari wa Nigeria walioko ughaibuni kurejea Nigeria
Kuhimiza makampuni ya kati na makubwa ya dawa kuongeza uzalishaji wa ndani wa dawa muhimu
Usalama
Kuboresha usajili wakati wa kuzaliwa ili kuwa na rekodi sahihi ya idadi ya watu na kuwezesha utambuzi bora wa uhalifu
Kuajiri hadi wafanyakazi milioni moja katika jeshi la polisi ili kufikia uwiano wa polisi wa Umoja wa Mataifa na raia wa 1:450
Kuboresha mahusiano ya kiraia na kijeshi
Kuunda upya na kugawanya taasisi za usalama
Elimu
Kukuza elimu ya sayansi na kiufundi ili kuunda ujuzi kwa uchumi mpya
Kuanzisha wakala wa kudhibiti elimu ya binafsi ya elimu ya juu
Kuongeza uwekezaji wa serikali kuu na za majimbo katika barabara, reli, umeme na nyumba
Rushwa
Kupitia mfumo wa malipo kwa wafanyakazi wa serikali
Kuweka mifumo ya kidigitali ya serikali ili kuongeza ugunduzi wa vitendo vya rushwa
Kuhakikisha kwamba hukumu za kesi za ufisadi zinatekelezwa na vyombo vinavyofaa
End of Uchaguzi Nigeria 2023: Vyama vinaahidi nini?