Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Anne Ali: Mwanamke wa kwanza mweusi kuwa Waziri Australia baada ya miaka 121
Serikali mpya imeundwa nchini Australia.
Mawaziri 23 katika baraza jipya la mawaziri waliapishwa Jumatano.
Kulikuwa na wanawake 10 katika baraza hilo la mawaziri.
Waziri wa Masuala ya Vijana Anne Ali na Waziri wa Viwanda Ed Hussein walikuwa mawaziri wa kwanza Waislamu nchini Australia.
Annie Ali, waziri wa kwanza mwanamke Mwislamu nchini Australia, aliapishwa akiwa ameshika Quran mkononi mwake.
Serikali mpya iliyoundwa nchini Australia inajumuisha watu wa jamii ya wenyeji na wawakilishi wa walio wachache.
Kwa hiyo, serikali hii ni mojawapo ya watu wa aina mbalimbali katika historia ya nchi hiyo.
Anne Ali, Mbunge kutoka Australia Magharibi, alikuwa mwanachama wa Chama cha Labour.
Tangu wakati huo amehudumu kama mwanachama wa muungano wa chama na kwa sasa ni waziri.
Alizungumza na vyombo vya habari baada ya kuapishwa. ''Sikuwahi kufikiria kuwa ningekuwa waziri katika maisha yangu,'' alisema.
Dk. Ali hapo awali alikuwa mwanamke wa kwanza kuwa Mbunge wa Kiislam nchini Australia.
Kwa sasa yeye ndiye waziri wa kwanza mwanamke Muislamu.
Ali alichaguliwa kwenye nafasi ya Cowan katika mpaka wa Perth.
Eneo hilo lilipewa jina la Edith Cowan, Mbunge wa kwanza mwanamke wa Australia.
Anne Ali alizaliwa Misri.
Alipokuwa na umri wa miaka miwili, familia yake ilihamia Chipping Norton, kusini-magharibi mwa Sydney.
Mnamo mwaka 2020, Anne Ali alirejelea unyanyasaji wa nyumbani aliopitia, akitaka kampeni ya kitaifa dhidi ya unyanyasaji wa nyumbani.
''Nilikuwa mvumilivu sana, nilitumia muda na nafsi yangu. Nilificha uchungu wangu kwa kutibu majeraha yaliyonipata. Nilikaa kimya, nilikaa kimya kwa muda mrefu. Nilivumilia maumivu na huzuni, ulikuwa uamuzi mgumu nilio nao. nikamuacha baada ya kuteseka na baba wa mtoto wangu.', Aliambia vyombo vya habari.
Anne Ali, 55, alifanya kazi kama profesa na mwalimu kabla ya kuingia katika siasa. Amekuwa akitafiti kuhusu ugaidi, Utafiti wake juu ya watoto kugeukia ugaidi ni muhimu kukumbuka.
Ana PhD kutoka Chuo Kikuu cha Edith Cowan.
Kabla ya kuingia katika siasa alikuwa na nyadhifa muhimu katika utawala wa Australia Magharibi.
Maisha ya Anne Ali ni ya kusisimua. Alilea watoto peke yake kwa muda na alifanya kazi kwa ujira mdogo sana. Anne Ali anapenda sana mitindo na [oa alifanya alishirikisha na uanamitindo.
Babake Anne Ali alisomea uhandisi wa nguo lakini hakuwahi kupata kazi katika fani hiyo.
Alikuwa akifanya kazi ya udereva wa basi.
Kuna Waislamu wapatao laki 6 nchini Australia.
Jumuiya ya Waislamu nchini Australia ina furaha kwamba Anne Ali ni waziri.
Shirikisho la Mabaraza ya Kiislamu ya Australia lilimwandikia barua ya kumpongeza kwa mafanikio yake.
Afisa wa Baraza la Kiislamu Kerr Trad alisema kuongezeka kwa Waislamu nchini Australia hadi nyadhifa za juu kunatuma ujumbe mzito.
''Mafanikio ya Ali yanatusaidia kuona uwakilishi wa kisiasa kama fursa ya kuhudumia jumuiya ya vijana wa Kiislamu nchini Australia,'' alisema.
Alisema ushindi huo unatuma ujumbe kwa watu wa Australia kwamba Waislamu pia ni sehemu muhimu ya jamii.