Misikiti 8 ya zamani iliosaidia kusambaza Uislamu yawekwa katika turathi za dunia

Chanzo cha picha, CORBIS/GETTY IMAGES
Misikiti minane nchini Ivory Coast, ambayo inaaminiwa kuwa muundo wake wa ujenzi ulianza wakati wa himaya ya Mali karne kadhaa zilizopita, imepewa hadhi ya kuwa urithi wa dunia na Unesco.
Majengo hayo ni "kielelezo cha ushahidi muhimu wa biashara baina ya maeneo ya sahara " iliyosaidia kueneza Uislamu na utamaduni wa Kiislamu, limesema Shirika hilo la Umoja wa mataifa kuhusu masuala utamaduni.
Umbo la misikiti hiyo ni mchanganyiko wa mitindo ya ujenzi wa misikiti ya Kiislamu na mitindo ya maeneo hayo.

Chanzo cha picha, CORBIS/GETTY IMAGES
Misikiti hiyo iliyoko katika miji ya Tengréla, Kouto, Sorobango, Samatiguila, M'Bengué, Kong, na Kaouara imehifadhiwa vyema na ni kati ya misikiti 20 mikubwa iliyosalia nchini Ivory Coast, ambako kuna mamia ya misikiti ambayo wakati mmoja ilisimama mwanzoni mwa karne ya 20, kulingana Unesco.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe
Kulingana na Unesco, walionyesha kielelezo cha usanifu wa majengo yaliyojengwa tangu karne ya 14 katika jiji la Djenné, ambalo ni sehemu ya himaya ya Mali.
Mtindo huo ulisambaa hadi Sudan katika karne ya 16 na kukarabatiwa ili kukabiliana na hali ya hewa ya unyevunyevu.
Misikiti nchini Ivory Coast ina mtindo wa kipekee ambao unadhaniwa kutengenezwa baina ya karne za 17 na 18 wakati wafanyabiashara wa kiislamu na wasomi walipowasili kutoka Himaya ya Mali kusini, wakipanua biashara katika maeneo ya njia ya Sahara.

Chanzo cha picha, AFP/GETTY IMAGES

Chanzo cha picha, AFP/GETTY IMAGES












