Familia ya Zindzi yapongezwa kwa kusema hadharani binti yao alikufa kwa Covid-19

2010 file picture of former South African President Nelson Mandela next to his daughter Zindzi (L) and fellow former political prisoner Ahmed Kathrada (R) in this handout photograph released by the Nelson Mandela Foundation

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Zindzi Mandela akiwa na baba yake Nelson Mandela 2010
Muda wa kusoma: Dakika 2

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amepongeza familia ya Rais wa kwanza wa nchi hiyo Nelson Mandela kwa kusema wazi kwamba binti yao, Zindzi, alikufa kwasababu ya ugonjwa wa virusi vya corona, Jumatatu.

Hilo litafanya jamii kutonyanyapaa wanafamilia waliopata maambukizi, Bwana Ramaphosa amesema.

Zindzi alizikwa Ijumaa asubuhi kando ya kaburi la mama yake ambaye pia alikuwa mwanaharakati aliyepinga ubaguzi wa rangi Winnie Madikizela-Mandela.

Afrika Kusini ni moja ya nchi za Afrika iliyopata maambukizi ya juu ya ugonjwa wa virusi vya corona ikiwa na zaidi ya maambukizi 320,000.

Kumekuwa na zaidi ya vifo 4,600 na serikali imekadiria kwamba idadi hiyo inaweza kuongezeka hadi 50,000 kufikia mwisho wa mwaka huu.

Licha ya kwamba raia wamefahamishwa kuhusu vile virusi vya corona vinavyosambaa, dalili na athari zake bado kumekuwa na taarifa za unyanyapaa dhidi ya waliopata maambukizi.

Rais Ramaphosa amesema nini?

"Ningependa kushukuru familia ya Mandela kwa mfano mzuri wa kushirikisha taarifa hizi na taifa. Hivi ni virusi ambavyo vinaathiri kila mmoja, na hakustahili kuwa na unyanyapaa wowote miongoni mwa waliopata maambukizi," alituma ujumbe kupitia mtandao wa Twitter kabla ya mazishi ya Zindzi Mandela.

Aliongeza kwamba kusema wazi sababu ya kifo chake, ni ishara ya mshikkamano wa juu zaidi kwa mwanamke aliyejitolea maisha yake kwa raia wenzake wa Afrika Kusini."

Presentational grey line

Pia unaweza kusoma:

Presentational grey line

Zindzi Mandela ni nani?

Zindzi Mandela, 59, alikuwa mtoto wa sita wa Nelson Mandela na Winnie Madikizela-Mandela, mke wake wa pili.

Waombolezaji waliokusanyika kwa ibada ya kumuaga Zindzi Mandela mjini Johannesburg walimpongeza kama mpiganiaji wa uhuru.

"Adui asiyeonekana ametupokonya baada ya Bi. Mandela hata baada ya kunusurika risasi, mateso na machungu aliyopata kwasababu ya mfumo wa ubaguzi wa rangi," Nomvula Mokonyane, afisa kutoka chama tawala cha African National Congress, amenukuliwa na tovuti ya shirika la habari la EWN.

"Alinusurika utawala wa kinyama kabisa miaka yake ya utotoni, na tulifikiria kwamba pia angenusurika janga hili na adui huyu asiyeonekana tunayekabiliana naye hii leo, kwasababu amepitia mabaya zaidi kuliko hili," amesema Julius Malema, kiongozi wa chama cha upinzani cha EFF, kulingana na taarifa.

Mourners are seen as the funeral procession carrying the body of Zindzi Mandela

Chanzo cha picha, Reuters

Maelezo ya picha, Waombolezaji walifika kwa ibada ua kumuaga Zindzi Mandela

Licha ya umaarufu wa baba yake, Bi. Mandela alikuwa mwanaharakati na alikuwa balozi wa Denmark hadi wakati wa kifo chake.

Alikua wakati wa enzi za ubaguzi wa rangi. Baba yake akiwa amefungwa gereza la Robben Island, alivumilia miaka mingi ya mateso na vitisho kipindi cha ubaguzi wa rangi, pamoja na dada yake Zenani na mama yake Winnie.

Maelezo ya video, What was apartheid? A 90-second look back at decades of injustice

Zindzi Mandela ndiye aliyesoma taarifa ya baba yake kukataa ombi la aliyekuwa Rais wakati huo, PW Botha aliyetaka Mandela aachiliwe huru kwa masharti katika mkutano wa hadhara Februari 1985.

Tazama:

Ruka YouTube ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa YouTube ujumbe

Presentational white space

Kupitia wakfu wake, aliyekuwa askofu wa mji wa Cape Town na mshindi wa Tuzo ya Nobel Desmond Tutu amesema kwamba "hotuba ya Soweto, kwa niaba ya baba yake... iliimarisha maadili na kanuni za kupigania ukombozi".

Bi. Mandela "alikuwa na jukumu muhimu kuashiria ubinadamu na kujitolea enzi ya ubaguzi wa rangi ", aliongeza.

Hivi karibuni alifahamika kwa kuunga mkono mabadiliko ya suala la ardhi Afrika Kusini.

Wawili tu kati ya watoto sita wa Nelson Mandela ndio ambao sasa hivi wako hai: Zenani Dlamini, dada ya Zindzi; na Pumla Makaziwe Mandela, binti wa ndoa yake ya kwanza, na Evelyn Mase.

Coronavirus
Banner