Je umewahi kuona nyani na simba pamoja?

Nyani akimlinda mwaka wa simba

Chanzo cha picha, Kurt Safari

Maelezo ya picha, Nyani akimlinda mwaka wa simba
Muda wa kusoma: Dakika 1

Afisa mmoja wa utalii nchini Afriika Kusini ambaye alifanikiwa kupata picha isio ya kawaida ya nyani akimbeba mwana wa simba katika mbuga ya kitaifa ya wanyamapori ya Kruger, amesema kwamba hajawaona tena wanyama hao tangu alipowapiga picha hiyo wiki iliopita.

Katika taarifa kwa BBC, mkurugenzi wa Kurt Safari , alisema kwamba msimu wa mvua umefanya kuwa vigumu kuwaona wanyama hao.

''Ni msimu wa mvua katika mbuga ya Kruger na miti imekuwa mikubwa huku nyasi zikiwa ndefu. Wakati nyani wanapoondoka katika barabara na kuingia katika nyasi , sio rahisi kuwaona''.

Ruka X ujumbe, 1
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 1

Picha hiyo ilileta shauku kubwa huku wengine wakisema kwamba ulikuwa ukweli wa filamu ya rafiki na simba.

Nyani akimbeba mwana wa simba katika mbuga ya Kruger Afrika kusini

Chanzo cha picha, Kurt Safari

Maelezo ya picha, Nyani akimbeba mwana wa simba katika mbuga ya Kruger Afrika kusini
Ruka X ujumbe, 2
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe, 2

Bwana Schultz alisema kwamba mwana huyo wa simba ambaye alikuwa amebebwa na nyani huyo alikuwa hatarini pengine.

''Nyani huyo wa kiume aliruka kutoka tawi moja hadi jingine akimbeba simba huyo mdogo kwa muda mrefu. Mwana huyo wa simba alionekana kuchoka na ijapokuwa hakuonekana kuwa na jeraha huenda alikua ameumia''.

''Nimeshuhudia nyani wakiwashambulia watoto wa chui na nimesikia nyani wakiwaua watoto wa simba lakini sijawahi kuona jinsi nyani anavyomlea vizuri mwana wa simba''.

Bwana Schultz aliongezea kwamba hadhani kwamba mwana huyo wa simba ataendelea kuishi.