Rushwa Kenya: Je kuziondoa noti za zamani zimesaidia kukabiliana na tatizo hili?

Old currency notes

Chanzo cha picha, AFP

Maelezo ya picha, Tarehe ya mwisho kuwasilisha noti za zamani ilikuwa Septemba 30
    • Author, Reality Check
    • Nafasi, BBC News

Tuhuma: Maafisa nchini Kenya wanasema hatua ya kuondoa matumizi ya noti za zamani katika jitihada za kukabiliana na rushwa au ufisadi imefanikiwa.

Uamuzi: Zaidi ya 96% ya noti hizo za zamani zimerudishwa na kubadilishwa kwa noti mpya, licha ya kwamba kuna shaka kuhusu ufanisi wa hili katika kubaini fedha zinazohusishwa na ufisadi. Hatua hiyo haionekani kuuathiri uchumi kwa ujumla kwa kiwango muhimu.

Presentational grey line

Gavana wa benki kuu Kenya Patrick Njoroge amesema shughuli ya kuziondoa noti hizo ilikwenda vizuri na wamefanikiwa kuzifanya fedha zinazomilikiwa na watu ambao hawakutaka zichunguzwe, kutokuwa na thamani.

Kati ya shilingi milioni 217 za noti za 1,000 zilizokuwa zikizunguka kuanzia Juni mosi wakati zoezi hili lilipotangazwa, milioni 210 million (96.6%) zilirudishwa kufikia Septemba 30.

Barclays bank branch Nairobi

Chanzo cha picha, Getty Images

Na hilo linamaanisha usawa wa $74m ziliishia kutokuwa na thamani.

Licha ya kwamba baadhi ya ambao bado wana noti hizo za zamani huenda wakawa:

  • wanaishi vijijini
  • wamekwama ng'ambo
  • wanaziweka kama kumbukumbu

Njoroge anaamini pia kuwa Kenya imeepuka matatizo yalioshuhudiwa India wakati mnamo 2016 taifa hilo liliondowa matumizi ya noti za thamani kubwa kama sehemu ya msako dhidi ya ufisadi na fedha haramu.

Ripoti ya benki kuu ya India imesema 99% ya noti hizo za zamani zilizokuwa ziktumia kabl aya marufuku ziliwasilishwa baadaye, kuashiria kuwa watu wengi waliokuwana fedha hizo kinyume cha sheria walifanikiwa kupata njia za kuzihifadhi kwenye benki kwa njia halali.

Visa 3,172 vya uzungukaji wa fedha vilivyotajwa kushukiwa wakati wa zoezi hilo nchini kenya vitachunguzwa, Njoroge anasema lakini 96% kati yao ulihusisha chini ya shilingi laki tano au $5,000.

Licha ya kwamba hili huenda pia likaashiria kuwa wale waliokuwa na fedha nyingi walifanikiwa kuzigawanya katika viwango vidogo vya fedha na kuepuka kuchunguzwa.

Nairobi supermarket aisles

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Kulikuwa na wasiwasi kwamba bei za bidhaa zingelipanda

Kwame Owino, wa taasisi ya masuala ya uchumi mjini Nairobi ameiambia BBC News: "Mojawapo ya sababu wa kuondolewa matumizi ya noti hizo - tunaarifiwa - ilikuwa ni haja ya kukabiliana na ufisadi na biashara haramu ya pesa, lakini hakuna aliyekamatwa kufikia sasa."

Na mwezi uliopita, benki kuu nchini iliripotiwa kuwa na wasiwasi kuhusu ongezeko la ghafla katika bei ya unga wa ngano katika sheemu moja nchini Kenya, huenda kutokana na watu wanaojaribu kukwepa udhibiti wa sarafu hiyo.

Overall annual inflation rate. . Overall year on year inflation rate in Kenya from September 2018 to September 2019 .

Kulikuwa na hofu pia kwamba zoezi hilo lingechangia wau kukimbilia kununua bidhaa, na kuchangia kuongezeka bei za bidhaa nchini.

Lakini hilo halikufanyika. Kiwango hicho kilishuka Septemba kwa 3.83%, kutoka 6.58% mnamo Aprili.

Baada ya mwezi wa kwanza kufuaia tangazo hilo, shilingi bilioni 25 ziliwekwa katika mabenki na kuchangia kushuka kwa kiwango cha fedha zilizo kwenye mzunguko nje ya mabenki.

Maafisa wanasema thamani ya sarafu ya shilingi ya kenya haikuathirika pakubwa.

Lakini imepanda kutoka 101.3 dhidi ya dola mapema Juni hadi 103.9 mwishoni mwa Septemba.

Noti hizo mpya pia zilinuiwa kuwa vigumu kutengeneza za bandia.

Lakini mwezi mmoja baada ya kuzinduliwa, washukiwa kadhaa walikamatwa na noti mpya feki.

Presentational grey line
Reality Check branding
Presentational grey line