Israel: Makaazi ya miaka 9000 yagunduliwa

Maelfu ya vitu, vito vya thamani, mbegu na vifaa vya kilimo vimepatikana katika eneo la jadi la makaazi yaliyodumu kwa miaka 9,000 nchini Israel.

Site of the Neolithic Period settlement near Jerusalem

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

Wana akiolojia wanaamini eneo hilo ambalo liko karibu na Motza, Magharibi mwa mji wa Jerusalem, wakati mmoja lilikua makaazi ya watu karibu 3,000.

Excavation works

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

Wachimbaji walipata mabaki ya jengo kubwa lenye vyumba kadhaa ambavyo watu walikua wakiishi wakati mmoja na kupata maeneo mengine ya matambiko yaliokua yakitumiwa na wakaazi hao.

Flint knife

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

Vitu vingine vilivyopatikana...

Spear head

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

...ni pamoja ncha ya mkuki uliyotumika kwa shughuli za uwindaji na pengine kujilinda.

Figurine of an ox

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

Vitu vingine vilipatikana ndani ya kaburi katika kile kinachoonekana kama vifaa vya kufanyia matambiko wakati wa kuzika.

Figurine, depicting a human face

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

White line 10 pixels

Jiwe hili kinaashiria kichwa cha binadamu.

Bracelet

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

Bangili tofauti zilizotengenezwa kutokana na mawe pia zilipatikana. Zilikua ndogo kuashiria kuwa zilikuwa zikivaliwa na watoto, watafiti wanasema.

Beads made of obsidian

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

Vifaa vingine vilivyopatikana glasi vilivyotokana na matope ya moto wa volkeno, kutoka Anatolia.

Excavation site

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

Mamlaka ya Israel inayosimamia vitu vya kale inasema uvumbuzi huo utabadilisha mawazo ya wanahistoria wa kale katika eneo hilo ambalo liliaminiwa kuwa makaazi ya Yudea enzi hizo.

Picha zote kwa hisani ya Mamlaka ya Israel inayosimamia vitu vya kale.