Israel: Makaazi ya miaka 9000 yagunduliwa
Maelfu ya vitu, vito vya thamani, mbegu na vifaa vya kilimo vimepatikana katika eneo la jadi la makaazi yaliyodumu kwa miaka 9,000 nchini Israel.

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority
Wana akiolojia wanaamini eneo hilo ambalo liko karibu na Motza, Magharibi mwa mji wa Jerusalem, wakati mmoja lilikua makaazi ya watu karibu 3,000.

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority
Wachimbaji walipata mabaki ya jengo kubwa lenye vyumba kadhaa ambavyo watu walikua wakiishi wakati mmoja na kupata maeneo mengine ya matambiko yaliokua yakitumiwa na wakaazi hao.

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority
Vitu vingine vilivyopatikana...

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority
...ni pamoja ncha ya mkuki uliyotumika kwa shughuli za uwindaji na pengine kujilinda.

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority
Vitu vingine vilipatikana ndani ya kaburi katika kile kinachoonekana kama vifaa vya kufanyia matambiko wakati wa kuzika.

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority

Jiwe hili kinaashiria kichwa cha binadamu.

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority
Bangili tofauti zilizotengenezwa kutokana na mawe pia zilipatikana. Zilikua ndogo kuashiria kuwa zilikuwa zikivaliwa na watoto, watafiti wanasema.

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority
Vifaa vingine vilivyopatikana glasi vilivyotokana na matope ya moto wa volkeno, kutoka Anatolia.

Chanzo cha picha, Israel Antiquities Authority
Mamlaka ya Israel inayosimamia vitu vya kale inasema uvumbuzi huo utabadilisha mawazo ya wanahistoria wa kale katika eneo hilo ambalo liliaminiwa kuwa makaazi ya Yudea enzi hizo.
Picha zote kwa hisani ya Mamlaka ya Israel inayosimamia vitu vya kale.












