Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ubalozi wa Marekani Tanzania watahadharisha Dar es Salaam kushambuliwa
Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania umetoa tahadhari kuwa kuna fununu za mipango ya mashambulizi jijini Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa tahadhari hiyo iliyochapishwa kwenye kurasa rasmi za mitandao ya kijamii ya Ubalozi huo, eneo la Masaki ndilo linalolengwa.
Eneo hilo lililopo kwenye rasi ya Msasani ni moja ya maeneo ya makazi ya kigahari zaidi jijini humo.
Tahadhari hiyo inabainisha kuwa, maeneo yanayolengwa ni mahoteli na migahawa ambayo hutembelewa na watalii ikiwemo eneo maarufu la maduka ya Slipway.
"Ubalozi hauna ushahidi wa moja kwa moja wa tishio hilo ama taarifa za muda gani mashambulizi yatatokea, hata hivyo unawaonya wananchi kuchukua tahadhari."
Tutaendelea kukujuza zaidi kadri tutakavyokwa tunapokea taarifa juu ya tahadhari hiyo.