Jay Z na Lady Gaga ni miongoni mwa wanamuziki waliosusia kushiriki katika filamu ya R. Kelly

Chanzo cha picha, Getty Images
Jay z na Lady Gaga ni mongoni mwa wanamuziki maarufu ambao walikataa kuonekana katika filamu inayoonyesha maisha halisi ya R.Kelly , mtayarishaji wa filamu hiyo ameeleza.
Makala hiyo ya 'Surviving R Kelly', ilizinduliwa jana nchini Marekani ikiwa imeangazia madai ya unyanyasaji wa kingono ambayo yamekuepo dhidi yake kwa miongo kadhaa ambapo amekataa kuusika na madai yote.
John Legend ni mwanamuziki pekee aliyekubali kuhojiwa .
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 1
Mwezi Desemba 2018, mfululizo wa Makala hiyo uliondolewa baada ya watu kuanza kupata simu za vitisho.
Muandaaji wa Makala hiyo , Dream Hampton alisema kuwa ilimuwia vigumu kupata watu mashuhuri kushirikiana na R.Kelly ili iweze kuendelea.
"Tulimuomba Lady Gaga , Erykah Badu ,Celine Dion, Jay-Z, Dave Chappelle na wote walikuwa muhimu kwake," lakini Hampton hakuhamini kwa nini hawakumuunga mkono yeye wala jitihada zake.

Chanzo cha picha, Getty Images
John Legend ndio mwanamuziki pekee ambaye alikubali kushiriki katika mfululizo wa Makala hiyo ambapo ataonekana katika mfululizo wa mwisho wa filamu hiyo utakaoneshwa kesho.
"R Kelly amesababisha maumivu mengi kwa watu," Hampton alisema.
Muimbaji ambaye alikuwa anasifika kwa uimbaji , Hampton alimuita 'shujaa' licha ya kuwa jina hilo alilikataa.
Kwa kila mtu kuniambia nilipata ujasiri gani kuonekana katika makala hiyo lakini mimi sikuona hatari yeyote",John alisema.
Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue
Mwisho wa X ujumbe, 2
Pamoja na kuwa mwanamuziki mwenye mafanikio makubwa katika historia ya muziki wa R&B, Kelly amekuwa akisakamwa kwa tuhuma za unyanyasaji wa ngono tangu mwaka 1990.
Makala hilo imefafanua uhusiano aliokuwa nao na mwanamuziki Aaliyah mwaka 1994, ambapo alimuoa Aliyah akiwa na umri wa miaka 15 wakati yeye akiwa na umri wa miaka 27.

Chanzo cha picha, Getty Images
Na badae jarida la Vibe lilibaini kuwa Aaliyah alikuwa amedanganya umri wake katika cheti cha ndoa kwa kuandika kuwa ana umri wa miaka 18.Ndoa hiyo ilifutwa mwezi Februari mwaka 1995.
Hivi karibuni mama yakeAliyah, Diane Houghton alitoa maoni yake alipohojiwa katika makala moja na kudai kuwa shutuma zote ni za uongo.
"Mume wangu alikuwa anasafiri na Aaliyah na alikuepo kwenye mahojiano yote na sehemu zote ambazo Aliyah alizuru kwa ajili ya muziki,"
Mfululizo wa filamu hiyo umeonyesha mke wa zamani wa R Kelly aiyejulikana kama Andrea, ambaye pia alitoa madai ya unyanyasaji.
Mwaka 2018, R Kelly alizindua wimbo wenye dakika 19 unaoitwa 'Admit' ambao ulijibu madai kadhaa dhidi yake dhidi ya ngono.












