Tsunami Indonesia: Picha zilizopigwa kwa juu zaonesha athari za tetemeko na hali ya manusura

Aerial view of a collapsed mosque amid rubble in

Chanzo cha picha, Reuters

Siku tano baada ya tetemeko kubwa la ardhi na tsunami iliyopiga mji wa Palu nchini Indonesian, picha hizi zinaonyesha hali halisi ya uharibifu uliotokea.

Before and after images of jetty in Palu

Kwa mujibu wa mamlaka ya maafa imeeleza kuwa idadi ya watu waliokufa katika eneo hilo inakadiriwa kuwa ,1300.

Chama cha msalaba mwekundu kimekadiria kuwa zaidi ya watu milioni 1.6 wameathirika wakati Umoja wa mataifa unasema kuwa ni watu wapatao 200,000 wana uhitaji wa haraka wa msaada.

Tathmini ya uharibifu inayoonyeshwa na ramani ya dharura iliyotolewa na Umoja wa ulaya inakadiria majengo 3,000 kuharibika katika janga hilo.

Map of Palu showing buildings damaged/destroyed in the tsunami

Watu wengi walikuwa ufukweni wakijiandaa kwa ajili ya tamasha wakati upepo mkubwa ulipopiga katika muda wa nusu saa au saa moja baada ya tetemeko la ardhi.

Debris litters the beach in Palu, Indonesia

Chanzo cha picha, Getty Images

Maeneo yote ya jirani kama Balaroa yametandwa na na matope.

Kuna baadhi wanakadiria kuwa nyumba 1,700 zilisombwa na upepo mkali mpaka Balaroa na nyingine mamia zilisombwa mpaka Petobo.

Miongoni mwa waliokufa 30 walikuwa wanafunzi katika kundi la kikristo la masomo ya biblia.

Mchanganyiko wa taka na mchanga uliongeza shinikizo lililotokana na tetemeko la ardhi uliosababisha mpasuko na kusomba majengo na miundombinu yake.

Images showing neighbourhood of Balaroa before and after mud inundation
Presentational white space

Eneo la mlimani liliachwa na matope na kusababisha udongo ushuke chini:

Aerial view of a collapsed hillside in Palu

Chanzo cha picha, Reuters

Tsunami imesababisha shughuli zote katika mji wa Palu kusimama.

Kuna uhaba wa chakula na maji ya kunywa pamoja na nishati.Udhibiti wa usafi wa mazingira ni tatizo linaloongezeka.Kuharibika kwa njia kunasababisha changamoto ya usafiri ambayo inakwamisha jitihada za uokoaji.

Jemalam bridge before the tsunami

Daraja la Jemalam lenye urefu w mita 126 na futi 410 ambalo linawakutanisha watu wapatao 350,000 wa upande wa magharibi na wale wa upande wa mashariki limeharibika.

Jemalam bridge after the tsunami has been destroyed

Watu wamekuwa wamekuwa wakiviokota vitu kwenye uchafu ili kupata chochote ambacho kinaweza kuwasaidia ili kufanya maisha yao yawe rahisi.

Overhead view of people looking through debris in Palu

Chanzo cha picha, Getty Images

Kwa sababu vitu kama makopo ya plastiki au vifaa vya vikoni ninaweza kuwasaidia

People on the roof of a collapsed building in Palu

Chanzo cha picha, AFP

Miili mingi ya waliokufa ilizikwa katika makaburi ya pamoja.Lakini inahofiwa kuwa kuna miili mingine ipo bado chini ya uchafu.

A man walks over the ruins of a building in Palu, Indonesia

Chanzo cha picha, Getty Images

Jeshi limechukua sehemu ya uwanja wa ndege ili kusafirisha misaada na watu walioumia sana.

Maelfu ya watu walikuwa wanasubiri ndege za kibiashara ili kuondoka katika mji huo wa Palu.

Soldiers watch as people board a military plane at Palu airport

Chanzo cha picha, Getty Images