Mgahawa wa Java House wabomolewa Kileleshwa, Nairobi

Java

Chanzo cha picha, HISANI

Muda wa kusoma: Dakika 1

Jengo lililo na mgahawa maarufu wa Java House katika mtaa wa Kileleshwa, Nairobi umebomolewa katika shughuli ya bomoa bomoa ambayo imeanza mapema leo asubuhi.

Shughuli hiyo inadaiwa kuendeshwa na Mamlaka ya Taifa ya Mazingira (Nema) na kulenga maeneo yaliyotengewa chemchemi za maji na kingo za mito.

Kituo cha mafuta cha Shell ambacho kinapatikana hapo karibu pia kimefungwa.

Mgahawa huo umeandika kwenye Twitter kwamba tawi lake la Kileleshwa limefungwa "kutokana na sababu zisizoepukika."

Ruka X ujumbe
Ruhusu maudhui? (Mitandao ya kijamii)

Mkala hii imebeba madhui yaliyotoka kwenye mitandao ya kijamii. Tunaomba ruhusa yako kabla kitu chochote hakija pakiwa, sababu wanaweza wakawa wanatumia Cookies na tekinolojia nyingine. Unaweza ukasoma sera sera ya kutumia cookies katika mitandao ya kijamii kabla ya kukubali. Kutazama maudhui haya chagua accept and continue

Onyo: Imetoka kwingine na inaweza kuwa na matangazo

Mwisho wa X ujumbe

Shughuli ya bomoa bomoa imekuwa ikiathiri watu wengi na sana wafanyabiashara wadogo ambao wamejenga vibanda vyao kando mwa barabara.

Maelfu ya wakazi katika mtaa wa Kibera, Nairobi pia waliathiriwa na ubomoaji ambao ulilenga kuondoa nyumba zilizojengwa katika eneo lililotengewa barabara ya mchepuko ya kuunganisha barabara za Langata na Ngong.

Maelezo ya video, Mamia ya wakaazi wa Kibera Kenya kupoteza makaazi yao katika bomoa bomoa