Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wanafunzi wasulubiwa na kutandikwa viboko kwa kuchelewa Nigeria
Watu watatu wamekamatwa Nigeria kwa kutuhumiwa kuwafunga wanafunzi katika misalaba na kuwatandika viboko barabarani.
Watu hao watatu - akiwemo mwalimu mkuu - wanazuiwa baada ya polisi kupita na kushuhudia kisa hicho kuisni magharibi mwa jimbo la Ogun.
Picha zinaonyesha watu wawili - mmoja mvulana na miwngine msichana - waliofungwa kwenye msalaba kwa kamba ya kijani.
Msemaji wa polisi ametaja adhabu hiyo kama ya 'kiunyama'.
Taarifa katika eneo hilo zinasema walikuwa wanaadhibiwa kwa kuchelewa shuleni.
Afisa huyo - anayefahamika kwa jina moja tu Livinus - alijaribu kuingilia kati, akimtaka mwalimu mkuu awaachie wanafunzi hao .
Na wakati mwalimu mkuu huyo alipokataa afisa aliamua kuchukua hatua na aksukumwa nyuma kwa nguvu.
'Nilipo jaribu kuwafungua wanafunzi , mwalimkuu na walimu wake walinipiga, aliliambia gazeti la Nigeria Punch. 'Kabla nirudi kutoka kwenye gari langu kuchukuwa pingu , walimshikilia rafiki yangu niliyekuwa naye..... na kumchapa kwa kiboko.'
Washukiwa hao hatimaye walikamatwa baada ya afisa wa polisi kupata usaidizi kutoka kwa maafisa wengine waliowasili.
Msemajiw a polisi katika jimbo la Ogun, Abimbola Oyeyemi ameithibitishia BBC kuwa mwalimu mkuu, mmiliki na mwalimu mwingine walikamatwa na huenda wakashtakiwa.
Aliongeza: "Hiyo sio kumuadhibu mtoto tena, ni unyama uiskubalika na hatuwezi kuuvumilia."