Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kwa Picha: Zaidi ya watu 40 wafariki mkasa wa bwawa Kenya
Watu zaidi ya 40 wamefariki baada ya bwawa moja kubwa katika shamba la kibinafsi eneo la Solai, Nakuru kaskazini magharibi mwa jiji la Nairobi kuvunja kingo zake.
Juhudi za uokoaji zinaendelea.
Bwawa hilo lilivunja kingo zake baada ya kujaa kutokana na mvua kubwa ambayo imekuwa ikinyesha katika eneo hilo na maeneo mengine Kenya.
Watu zaidi ya 100 kufikia sasa wamefariki nchini Kenya kutokana na mafuriko ambayo yameathiri pia nchi jirani kama vile Tanzania, Uganda, Somalia na Ethiopia.
Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya limekuwa likisaidia na maafisa wa huduma za dharura wa serikali na wahudumu wa kujitolea kuwasaidia waathiriwa.
Hapa chini ni baadhi ya wakazi walionusurika wakiwa ndani ya gari la kuwabebea wagonjwa.
Bwawa hilo linapatikana eneo la Solai, wadi wa Kabazi kilomita 40 hivi kaskazini mwa mji wa Nakuru.