Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Utafiti: Ngono haichangii sana mshutuko wa moyo
Mshutuko wa ghafla wa moyo unaotokana na tendo la ngono unaweza kutokea zaidi miongoni mwa wanaume kuliko kwa wanawake, kwa mujibu wa utafiti.
Lakini hata hivyo pia kuna uwezekano mdogo kwa ngono kusababisha mshutuko wa moyo
Ni asilimia 34 ya visa 4,557 vya mshutuko wa moyo vilivytokea wakati wa tendo la au baada ya saa moja ya ngono na 32 kati ya wale walioathiriwa walikuwa ni wanaume.
Dr Sumeet Chugh, kutoka taasisi ya moyo ya Cedars-Sinai, anasema utafiti huo ndio wa kwanza kubaini ikiwa tendo la ngono linaweza kusababisha mshtuko wa moyo.
Hali hiyo hutokea wakati moyo unakumbwa matatizo na kuacha kupiga.
Dr Chugh na wenzake huko California walikagua rekodi za hospitali kuhusu kesi za mshutuko wa moyo kwa watu wazima kati ya mwaka 2002 na 2015 huko Portland, Oregon.
Ngono ilichangia chini ya asilimia moja ya visa hivyo. Wengi walikuwa ni wanaume walio katika umri wa makamo.