Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Wadukuzi wa Korea Kaskazini waliiba siri za kijeshi za Korea Kusini
Wadukuzi kutoka Korea Kaskazini walidukua mitambo ya kijeshi ya Korea Kusini na kuiba nyaraka nyingi zenye taarifa muhimu za kijeshi.
Miongoni mwa yaliyokuwemo kwenye nyaraka hizo ni mpango wa kumuua kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un.
Mbunge wa Korea Kusini Rhee Cheol-hee amesema taarifa hizo zilitoka kwa wizara ya ulinzi ya Marekani.
Nyaraka hizo zilikuwa na mipango ya karibuni zaidi ya kijeshi kati ya Korea Kusini na Marekani.
Korea Kusini mwezi mei ilifichua kwamba sehemu kubwa ya data iliibiwa na wadukuzi Septemba mwaka jana, madai ambayo Korea Kaskazini ilikanusha.
Jeshi la Korea Kusini limesema kufikia sasa asilimia 80 ya taarifa ambazo ziliibiwa kufuatia udukuzi huo bado hazijatambuliwa.