Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Trump aizungumzia Texas
Rais Donald Trump ameahidi kuliunga mkono jimbo la Texas katika kipindi hiki ambacho kimbunga Harvey kinaendelea kuharibu eneo hilo.
Wakati akijiandaa kwenda katika jimbo hilo leo, amesema kuyalinda maisha ya watu kutakuwa ni kipaumbelke cha kwanza kwake.
Amesema mchakato wa kulijenga tena eneo hilo utakuwa ni kazi ya muda mrefu na ngumu.
Mamilioni ya dola za Kimarekani zinahitajika, huku bunge la nchi hiyo la Congress likihitajika kuidhinisha fedha hizo.