Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Meneja wa teknolojia wa tume ya uchaguzi Kenya atoweka
Tume huru ya uchaguzi na mipaka nchini Kenya IEBC, imesema kuwa mmoja wa mameneja wake wa masuala ya teknolojia hajulikani aliko.
IEBC inasema kuwa mtu huyo alionekana mara ya mwisho siku ya Ijumaa jioni.
Mawasiliano ya mwisho kutoka mwa mtu huyo aliyafanya siku ya Jumamosi mwendo wa saa tisa alifajiri kupitia ujumbe wa SMS na mmoja wa wafanyakazi wenzake.
Aliyoandika kwenye ujumbe huo yalionyesha kuwa alikuwa akijielewa na alikuwa na mipango ya siku.
Ripoti tayari imepelekwa kwa polisi huku IEBC, familia yake na pia polisi wakishirikiana kujaribu kubainia aliko.
Kisa hiki kinatokea ikiwa imesalia juma moja kabla ya kufanyika kwa uchaguzi mkuu nchini Kenya ambao utafanyika tarehe 8 Agosti.