Mtu tajiri zaidi barani Asia Jack Ma ziarani Kenya

Jack Ma

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Jack Ma

Mtu tajiri zaidi barani Asian Jack Ma, yuko nchini Kenya wakati anapoanza ziara yake katika nchi za Afrika Mashariki.

Bwana Ma ambaye anamiliki kampuni ya Alibaba ambayo inaripotiwa kumiliki asilimia 11 ya biashara ya mtandao nchini China, atawahutubia vijana mjini Nairobi kabla ya kuelekea nchini Rwanda kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa.

Anaoandamana nao katika ziara hiyo ni kundi la wafanyabiashara matajiri wa kichina ambao wanatafuta fursa za uwekezaji.

Kampuni ya Alibaba inaripotiwa kumiliki asilimia 11 ya biashara ya mtandao nchini China

Chanzo cha picha, Getty Images

Maelezo ya picha, Kampuni ya Alibaba inaripotiwa kumiliki asilimia 11 ya biashara ya mtandao nchini China