Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mtu tajiri zaidi barani Asia Jack Ma ziarani Kenya
Mtu tajiri zaidi barani Asian Jack Ma, yuko nchini Kenya wakati anapoanza ziara yake katika nchi za Afrika Mashariki.
Bwana Ma ambaye anamiliki kampuni ya Alibaba ambayo inaripotiwa kumiliki asilimia 11 ya biashara ya mtandao nchini China, atawahutubia vijana mjini Nairobi kabla ya kuelekea nchini Rwanda kuhudhuria mkutano wa Umoja wa Mataifa.
Anaoandamana nao katika ziara hiyo ni kundi la wafanyabiashara matajiri wa kichina ambao wanatafuta fursa za uwekezaji.