Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kiongozi wa kundi la mihadarati Mexico akamatwa
Mamlaka nchini Mexico imesema kuwa imefanikiwa kumtia nguvuni mmoja wa wanachama wa Saniola kundi ambalo awali lilikuwa likiongozwa na mfanya biashara maarufu wa dawa za kulevya Joaquin Guzman akijulikana zaidi kama ''el Chapo''.
Damaso Lopez alikamatwa katika mji wa Mexico City kwa tuhuma za kusafirisha tani za dawa za kulevya kwenda Marekani.
Tokea kukamatwa kwa aliyekuwa kiongozi wao Joaquin Guzman, viongozi wa juu wa Saniola wamekuwa wakihitilafiana kwa kung'ang'ania madaraka hali iliyopelekea kuibuka kwa uhalifu katika maeneo ya Saniola.