Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Kifo cha Kim Jong Nam: Malaysia yalaani utumizi wa kemikali
Malaysia imelaani utumizi wa silaha ya kemikali iliyotumika kumuua Kin Jong Nam ambae ni kaka wa kambo wa kiongozi wa Korea Kaskazini katika uwanja wa ndege wa Kuala Lumpur mwezi uliopita.
Malaysia hata hivyo haijahusisha Korea Kaskazini na mauaji hayo lakini taarifa ya wizara ya mambo ya nje imeelezea wasi wasi wake kutokana na utumiaji wa kemikali hiyo ambayo ilihatarisha maisha ya raia wengi.
Taarifa hio imejiri saa chacha baada ya Korea Kaskazini kupinga matokeo ya upasuaji wa maiti uliofanywa na maafisa wa Malaysia na kupata kwamba Kemikali ya VX ilitumika kumuua Kim Jong Nam.