Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Miili ya wahamiaji 74 yasombwa hadi fukwe za Libya
Shirika la hilali nyekundu nchini Libya linasema kuwa limepata miili ya wahamiaji 74, ambayo ilisombwa hadi fukwe zilizo karibu na mji wa magharibi wa Zawiya.
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM, lilisema kuwa wahamiaji hao walikuwa kwenye mashua ambayo iliondoka nchini Libya siku ya Jumamosi ikiwa na watu 110.
Maiti hizo zitazikwa mjini Tripoli kwenye makaburi ya watu wasiotambuliwa.
Hivi majuzi Muungano wa Ulaya ulikubali kutoa msaada wa dola milioni 215 kwa serikali inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa kupunguza idadi ya wahamiaji.
Mwaka uliopita wahamiaji 5000 walizama maji walipojaribu kufika ulaya wakipitia bahari ya Mediterranean.