Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Israel kujenga nyumba 560 kwa walowezi mashariki mwa Jerusalem
Wakuu wa Israel wameidhinisha ujenzi wa nyumba 560 kwa ajili ya walowezi, mashariki mwa Jerusalem.
Naibu wa meya wa Jerusalem Meir Turjeman, alisema idhini hiyo ilichechelewa kufuatia ombi la waziri mkuu, Benjamin Netanyahu, baada ya azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, lilopinga ujenzi wa makaazi hayo.
Marekani haikupinga azimio hilo kwa kura yake ya turufu.
Wapalestina wanatumai kuwa Jerusalem Mashariki itakuwa mji mkuu wa taifa lao litakapoundwa siku za mbele.