Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Barrow amtaka Jammeh kushiriki mazungumzo
Mshindi wa Uchaguzi wa Rais nchini Gambia Adama Barrow amemtaka Rais anayemaliza muda wake Yahya Jammeh kushiriki katika mazungumzo ya moja kwa moja ili kutatua mgogoro wa kisiasa ulioikumba nchi hiyo.
Katika Mahojiano na BBC, Barrow amesema anauhakika kwamba ataapishwa kama kiongozi mkuu wa taifa hilo wiki ijayo, licha ya Rais Jammeh kukataa kukubali kushindwa katika uchaguzi huo uliofanyika mwezi uliopita.
Wasuluhishi kutoka Jumuia ya Uchumi ya nchi za Afrika Magharibi ECOWAS wanatarajiwa kuwasili Gambia baadaye leo katika jaribio lingine la kumtaka Rais Jammeh kukubali kuondoka madarakani, wakati awamu yako itakapomalizika Jumatano wiki ijayo.
Iwapo atakataa viongozi hao wa ECOWAS wamesema watazingatia kumuondoa kwa nguvu madarakani.
Rais Jammeh amepeleka shauri mahakamani kupinga matokeo ya uchaguzi huo.