Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
China yakamata chombo cha Marekani baharini
Marekani imetoa ombi kwa China ikiitaka iwachilie chombo cha baharini ilichokamata katika maeneo ya bahari ya kimataifa.
Jeshi la wanamaji wa China lilikamata chombo hicho cha utafiti wa chini ya bahari, kusini mwa bahari ya China siku ya Alhamis.
Kisa hicho kilitokea wakati meli moja ya Marekani ilikaribia kukiondoa chombo hicho baharini
Chombo hicho kwa jina "naval glider" kinatumiwa kufanyia utafiti viwango vya chumvi baharini na pia vya joto.
"Chombo hicho kilikuwa kikiendesha utafiti kulinga na sheria za kimataifa kusini mwa bahari ya China,"maafisa wa Marekani walisema.