Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Syria: Mapigano yaisha Mashariki mwa Aleppo
Operesheni za kijeshi zimemalizika mashariki mwa mji wa Aleppo, Balozi wa Urusi ndani ya Umoja wa Mataifa , ameeleza.
Vitaly Churkin amesema Serikali imeweza kudhibiti maeneo yaliyokuwa yamebaki mikononi mwa waasi.
Tangazo hilo kama litathibishwa, litakuwa limemaliza mapigano yaliyodumu kwa zaidi ya miaka minne.
Awali, bwana Churkin alisema mipango inapangwa ili kuwaondoa waasi kwenye mji huo, Waasi wameridhia mpango wa kuondoka.
Makubaliano hayo yamekuja wakati ambao Umoja wa mataifa ukitoa ripoti ya mauaji yaliyotekelezwa na vikosi vya serikali ya Syria.
Ofisi ya umoja wa mataifa inayoshughulikia masuala ya haki za binaadam imesema ina ushahidi wa kuaminika kuwa katika maeneo manne raia 82 waliuawa, na kuongeza kuwa watu zaidi wameuawa.