Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Trump aendelea na uteuzi wa viongozi mbalimbali kwenye utawala wake
Ikiwa imebakia miezi miwili kabla ya kuapishwa rasmi kuwa Rais wa Marekani, mwishoni mwa wiki Donald Trump amerejea mjini New York akiendelea na mfululizo wa vikao vya uteuzi wa nafasi mbalimbali katika utawala wake.
Trump amekutana na mpizani wake Rick Perry aliyekuwa gavana wa jimbo la Texas.
Trump anatarajiwa pia kukutana na Tulsi Gabbard ambaye ni mbunge mwanamke wa chama cha Democratic aliyekuwa akimuunga mkono Bi Hillary Clinton ambapo kiongozi huyu ndiye mwanamke pekee mwenye asili ya kihindi aliyewahi kuchaguliwa kuwa mbunge nchini marekani.
Msemaji wa Trump Kellyanne Conway amesema kuwa Bwana Trump anataka kusikia mawazo tofauti tofauti kutoka vyama vingine.