Wasanii Sudan kusini wachora kushinikiza amani Juba

Baada ya vita vya takriban miaka mitatu, wasanii Sudan kusini wameshirikiana katika kujaribu kuishinikiza nchi kukaa pamoja na kujadili amani, kwa kuanzisha michoro katika maeneo ya umma mjini Juba.

Baada ya kusambaza ujumbe wake katika baadhi ya kuta za mji wa Juba, kundi hilo sasa linapanga kupanua mradi wake nje ya mji mkuu huo.