Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mawakili wasema hawatamtetea mshukiwa wa Paris
Mawakili wa mshukiwa mkuu wa shambulio la kigaidi lililotekelezwa mjini Paris Novemba mwaka jana, Salah Abdeslam, wamesema hawatamtetea tena.
Abdeslam anapanga kutumia haki yake ya kukaa kimya kortini, mmoja wa mawakili wake, Frank Berton, ameambia BFM TV.
"Tulisema tangu mwanzo ... kwamba mteja wetu akiamua kukaa kimya tutajiondoa," amesema, akiwa ameandamana na wakili mwenzake Sven Mary.
Watu 130 waliuawa wakati wa mashambulio hayo.
Kundi linalojiita Islamic State limedai kuhusika.
Salah Abdeslam alikamatwa mjini Brussels mwezi Machi na amesalia kimya tangu alipohamishiwa Ufaransa mwezi Aprili.