Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Ethiopia yatangaza hali ya tahadhari ya miezi 6
Serikali ya Ethiopia imetangaza hali ya dharura kwa miezi sita.
Tangazo hilo limetolewa baada ya miezi kadha ya maandamano dhidi ya serikali, yaliyofanywa na makabila mawili makubwa ya Ethiopia ya Oromo na Amhara.
Makabila hayo yanalalamika kuwa yametengwa kiuchumi na kisiasa.
Ghasia baina ya waandamanaji na polisi zilizidi tangu watu 55 walipokufa katika sherehe za kitamaduni za Oromo, Jumapili iliyopita.
Mashirika ya kutetea haki za kibinaadamu yanasema, mamia ya watu wameuawa, na maelfu kukamatwa tangu maandamano yalipoanza