Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Mwanazuoni wa Iran aachiliwa gerezani
Shirika la habari la Iran linasema kuwa mwanamke mmoja mwanazouni mzaliwa wa Iran mwenye asili ya Canada ameachiliwa huru kutoka gerezani kwa misingi ya kibinaadam.
Homa Hoodfar, Profesa mstaafu alikamatwa mjini Tehran mwezi Juni.
Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ameliambia shirika hilo la habari kwamba mwanamama huyo ameachiliwa huru kutokana na sababu za maradhi, na kwamba alikuwa njiani kurudi Canada akipitia oman.
Familia ya Bi Hoodfar inasema kuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa mishipa ya fahamu.
Mwanazuoni huyo mstaafu alikuwa ni mmoja ya watu wengi wenye uraia pacha amabo wanashikiliwa nchini iran kwa tuhuma za vitendo vya kuhatarisha usalama wa taifa.