Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Jumba la kumbukumbu za Wamarekani weusi lafunguliwa US
Rais wa Marekani Barrack Obama amefungua rasmi jumba la kumbukumbu za Wamarekani-weusi mjini Washington DC.
Obama amesema kuwa jumba hilo la utamaduni na historia ya Wamarekani weusi litatoa historia ya Marekani ambayo haijatambuliwa na wengi.
Mtindo wa Jumba hilo ulichorwa na raia wa Uingereza David Adjaye.
Huku baadhi ya vitu vilivyopo katika jumba hilo vikionyesha wakati wa utumwa, vyengine vinaonyesha utamaduni wa watu weusi ambao umeingia katika utamaduni wa Marekani.
Wanaharakati wa haki za watu weusi nchini Marekani walipendekeza kujengwa kwa jumba hilo mwaka 1915.