Hii ni tovuti ya maandishi pekee ambayo inatumia data kidogo. Tazama toleo kuu la tovuti likijumuisha picha na video zote.
Pata maelezo zaidi kuhusu toleo hili la linalotumia kiasi kidogo cha data
Somalia imekabiliana na Kenya katika mahakama ya Hague
Katika mahakama The Hague, Somalia imejibu shutuma kutoka Kenya katika mzozo wa ardhi, shirika la habari la AFP linaripoti.
Mataifa hayo mawili yamekuwa yakikabiliana kisheria katika mahakama ya kimataifa ya haki (ICJ) kuhusu eneo uliopo mpaka wa baharini baina ya nchi hizo mbili.
Somalia inasema Kenya inarefusha pasi sababu mzozo huo wa umiliki wa bahari inayoaminika kuwa na utajiri wa mafuta na gesi, AFP inaripoti.
Jumatatu, Kenya imetaja tuhuma za Somalia kuwa inataka kuiba akiba ya mafuta na gesi katika eneo hilo, kama ''tuhuma za kutia uchungu na zisizo za kweli".
Somalia inasema imewasilisha kesi hiyo katika mahakama ya ICJ baada ya kujaribu na kushindwa kujadiliana na Kenya.